0


Business Decision
Mojawapo ya swali kubwa ambalo watu wengi wanajiuliza kila mara ni kuwa, ni hatua gani muhimu anayoweza mtu yoyote kuichukua ili kuweza kufikia katika eneo la kutengeneza mafanikio yake? Hii inaonyesha ni jinsi gani watu wengi wanavyojaribu kutafuta njia yoyote ya kufanikiwa kwa gharama yoyote ile hata kama ni kwa njia ya mkato ilimradi kufikia katika mafanikio, na kumbuka mafanikio ya kweli hayana njia ya mkato. Kadiri unavyochukua hatua ya kivitendo pasipo uoga, ndio kadiri unavyozidi kuongeza nafasi ya kwenda katika mafanikio unayoyahitaji.
Nidhamu yako, uwezo wa kutokubadilika badilika katika kufaata maamuzi yako na kutokukata tamaa katika hatua uliyoamua kuichukua katika kufuata ndoto yako, hizi ndio tabia pekee zinazoweza kukujengea kujiamini na kufanikiwa haraka ukiunganisha na mambo mengine bora unayoweza kuyatumia katika kufanikisha ndoto na malengo yako uliyonayo katika maisha.
Ni vizuri ufahamu ni namna gani ya kuchambua na kupigia hesabu kamili ya kiasi gani cha muda na hatua maalum unazotakiwa kuzichukua ili kujenga mawazo mapya, kujiamini na kuvumbua mambo mapya yatakayokusaidia katika kutengeneza mipango yako mizuri ya kufikia katika mafanikio makubwa.
Watu wengi wanafeli na kushindwa kabisa ni kwa sababu wanashindwa kuchukua hatua sahihi zinazoweza kuwapeleka katika kuchukua vitendo timilifu vya kuwapeleka katika mafanikio yao. Unapohitaji kuchukua hatua za kivitendo katika jambo lolote lile la mafanikio ni uamuzi wa kwako kufanya uchaguzi katika nganzi hizi nne.
1: Kutokuamua kufanya chochote au kutokuamua kuchukua hatua kabisa.
Si uongo kwamba kuchukua hatua ya kivitendo ndio jambo pekee linaloweza kuwa chachu ya mtu yoyote kufanikiwa katika malengo na mipango yake aliyonayo. Uamuzi wa kuchukua hatua au kutokuchukua hatua katika kufuata njia yako ya mafanikio upo juu yako tofauti na unavyofikiri, wewe ndiye mwenye uamuzi wa mwisho juu ya kufanikisha ndoto yako. Watu wengi ambao wameshindwa kuona matokeo yoyote katika taaluma zao, biashara, mahusiano, nakadhalika, hii ni kwa sababu wengi wao si watu wa kuchukua hatua zinazostahiri kwa ajili ya kufikia ndoto zao nzuri walizonazo.
Yawezekana ni mmojawapo wa watu wenye kupanga malengo na mipango mingi ya kufikia ndoto yako, lakini si mtu uliye mwepesi wa kuchukua hatua ya juu za kivitendo, nataka nikuambie ni ngumu sana kufanikiwa na kufikia hatima ya ndoto yako. Kutokuamua kufanya chochote juu ya mipango na malengo yako uliyonayo ni uamuzi ulio ndani yako binafsi na mwenye uwezo wa kuubadili wewe pekee. Uamua kubadilika na kukimbia uamuzi huu husio mzuri wa kutokuchukua hatua za kivitendo kabisa katika malengo na mipnago yako mizuri uliyonayo.
2: Kuamua kurudi nyuma.
Mara nyingi hatua hii hutokea pale mtu anapojaribu kutimiza malengo au jambo fulani lenye mafanikio kwake binafsi na pale linapotokea jambo gumu au zito mbele yake kama changamoto uamua kurudi nyuma au kukata tamaa au kukimbia tatizo badala ya kulikabili. Mtu huyu ninaweza kumwita ni mtu aliye mwoga wa kukabili changamoto, huku pasipo kujua kupitia changamoto huwezi kufikia kufanikiwa kwa kiwango unachokitaka.
Watu wengi wanaorudi nyuma kwa ajli kutimiza ndoto zao kwa uoga wa jambo fulani linalowakabili mara nyingi huwa ni watu wa kutoa visingizio juu ya hatua waliyoamua kuichukua ya kurudi kwao nyuma. Ni watu wanaotumia muda mwingi kutoa sababu juu ya kwa nini hatua waliyoichukua na kwa nini wameamua kurudi nyuma kufanya jambo fulani. Nakusihi husiwe miongoni mwa watu wanaotoa sababu na watu wanaorudi nyuma mara kwa mara kwa sababu ya uoga bali amua kwenda mbele kwa ajili ya kufikia ndoto na maono yako.
3: Kuchukua hatua ya kiwango cha kawaida au kati.
Watu wengi walioamua kuchukua kiwango cha kawaida cha kutimiza malengo na mipango yao waliyonayo, watu hawa kwa idadi yao ni wengi na tena ni kubwa sana katika jamii yetu ya leo. Hili ni kundi la watu ambalo kwa makusudi kabisa au kwa kutokujua limeamua kujikita kuchukua hatua za kivitendo kwa kiwango cha kati au kawaida tena wakati mwingine kwa kujiurumia binafsi tofauti na ndoto zao zinavyowataka. Huwezi kufanikiwa kwa kiwango cha juu, huku unachukua uamuzi wa kivitendo wa nganzi ya chini au kawaida, kwamwe hutoweza kufikia mafanikio makubwa unayoyataka.
Mara nyingi kundi la aina hii la watu ndio linalotengeneza maisha ya watu wenye uchumi wa kati (middle class people) katika jamii inayotuzunguka, watu hawa ndio wenye maisha ya kawaida katika ndoa, taaluma, mafanikio kifedha, nakadhalika; watu hawa hawafanikiwi zaidi kwa sababu si watu wenye kujituma zaidi na kuongeza bidii fulani katika kujiletea mafanikio yao halisi na ya kweli ambayo hata Mungu ameyakusudia juu yao. Usikubali kuishi maisha ya chini ya kiwango chako cha mafanikio hasa kwa kutenda mambo kwa namna ya kawaida, ongeza bidii ili ufikie hatua ya juu ya mafanikio yako.
4: Kuchukua hatua ya kiwango cha juu kabisa.
Hii ndio hatua ya juu ambayo kila mtu anatakiwa kuichukua katika kutimiliza malengo na mipango yake ili kuweza kufikia ndoto na maono yake aliyonayo. Angalia kwa mfano maisha ya watoto wadogo waliokuzunguka, mtoto yoyote mdogo huwa anatenda au kuchukua hatua ya kufanya vitendo vya hatari tena vikubwa ambavyo vinaweza kuwa hatarishi kwake, lakini kama hasipopata mtu wa kumwambia basi uendelea kufanya kitendo hicho. Hata mimi nakumbuka nikiwa mdogo kama miaka 7 hadi 10, nilikuwa katika hali ya namna hiyo, ni kwa nini? Ni kwa sababu mtoto mdogo hajui ubaya wa jambo lolote analolifanya; ila sasa ni kwa nini afanye vitendo vikubwa vya namna hiyo na huo ujasiri unatufundisha nini kwetu sisi kama watu wazima?
Nataka nikuambie kuchukua hatua ya kivitendo kwa kiwango cha juu kunahitaji ujasiri wa hali ya juu ili uweze kufanikiwa, kwa kuwa wengi wameogopa kutenda mambo makubwa kwa hofu ya kuumia, kuabika, kupoteza fedha, kupoteza heshima, nakadhalika. Lakini nataka ufahamu kuwa uamuzi wa kuchukua hatua hii kwa uaminifu ili kuyafaata mafanikio yako na kuifikia ndoto yako ni jambo bora zaidi kuliko kubaki katika hatua nyingine nilizotoka kuzielezea hapo juu.
Watu hawawezi kufahamu kipaji na uwezo wako ulionao kama hautoamua kuchukua hatua ya kivitendo ya kiwango cha juu tena kwa bidii ili kuwafikia watu wengi kwa namna chanya ambayo itawagusa watu hao kwa stahiri ya ajabu na wengi kukufahamu au kukutafuta kwa ajili ya kupata msaada kutoka kwako. Kama ni kampuni haiwezi kuwafikia wateja wengi kwa bidhaa na huduma zake kama haitohakikisha inatoa nguvu ya ziada ya kuchukua hatua ya juu ya kivitendo kwa ajili ya kufanikisha malengo na mikakati yake.
Hatua hii ya nne ndio imezaa mamilionea na mabilionea wengi unaowaona leo hii katika dunia, unasubiri nini kwako wewe na mimi kuwa katika hatua hii na kuchukua hatua ya kivitendo vya viwango vya juu ili kuwa sehemu ya mafanikio makubwa kama wengine. Nakuambia inawezakana kufanikiwa na mimi nimeanza muda kutekeleza hatua hii na sasa nakula matunda yake na bado sichoki kuchukua hatua hii hadi niifikie ndoto yangu ya kweli. Amua nawe kuwa miong

Post a Comment

 
Top