HALMASHAURI
ya wilaya ya Singida, imekusanya zaidi ya shilingi 67 milioni kwenye
harambee ya madawati iliyofanyika kwenye bwalo la shule ya sekondari ya
Mwenge mjini hapa.
Kati
ya fedha hizo,shilingi 10,006,500 ni fedha taslimu na ahadi ni shilingi
15,529,500. Aidha jumla ya madawati 754 yenye thamani ya shilingi
41,470,00 yalitolewa/yalichangwa kwenye harambee hiyo ambayo mgeni rasmi
alikuwa mbunge wa jimbo la Singida kaskazini Lazaro Samwel Nyalandu.
Nyalandu
amechangia madawati 100 yenye thamani ya shilingi 5.5 milioni kutoka
kwenye mfuko wake binafsi,kampuni ya simu ya halotel shlingi milioni
moja,kampuni ya Victoria enterprises, shilingi milioni 1.1,shirika
lisilo la kiserikali la Waendelee Wirwana madawati 500 yenye thamani ya
shilingi 27.5 milioni na mbunge wa viti maalum mkoa wa Singida,Ashyrose
Matembe amechangia madawati 50 yenye thamani ya zaidi ya shilingi 2.7
milioni.
Akizungumza
kwenye harambee hiyo iliyofana,Nyalandu pamoja na kuwashukru wadau
mbalimbali waliochangia kwenye harambee hiyo,amewataka wasichoke
kuchangia sekta hiyo ya elimu,ili shule za msingi na sekondari ziweze
kuwa na mazingira mazuri ya kufundishia na kujifunzia.
“Lengo
la halmshauri yetu ni kwamba kabla ya juni 30 mwaka huu,pasiwepo na
mwanafunzi anayekaa chini sakafuni au kwenye matofali wakati
akisoma.Agizo la rais wetu Magufuli tutalitekeleza kabla ya kumalizika
kwa muda alioupanga”,alisema Nyalandu kwa kujiamini.
Mkurugenzi
Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Singida, Simion Mumbee,akizungumza
kwenye harambee ya kuchangia madawati iliyofanyika mjini Singida. Zaidi
ya shilingi milioni 67 zilichangwa kwenye harambee hiyo.
Aidha,alisema
baada ya kujitosheleza kwa madawati,wataelekeza nguvu zao katika
kujenga nyumba bora za kuishi walimu wa shule za msingi na sekondari,ili
pamoja mambo mengine,ili kuwavutia walimu kuja kufundisha katika
halmashauri hiyo.
“Katika
halmashauri yetu,tunataka ifike siku wanafunzi wote wa shule za msingi
na sekindari wawe na madawati,hali kadhalika walimu wote wawe na nyumba
bora za kuishi zilizojitosheleza kwa kila kitu muhimu
kinachohitajika”,alisema.
Awali
afisa elimu wa sekondari,Dorothy Kobelo, alisema halmashauri hiyo
imejiwekea mikakati mbalimbali katika kukabiliana na upungufu wa
madawati kwa, lengo la kutekeleza agizo la rais Magufuli kwamba ifikapo
juni 30 mwaka huu,kusiwepo na wanafunzi anakaa sakafuni wakati wa
kusoma.
Afisa
elimu sekondari halmashauri ya wilaya ya Singida, Dorothy Kabelo,
akitoa taarifa ya upungufu wa madawati katika shule za msingi na
sekondari katika halmashauri hiyo. Halmashauri hiyo inakabiliwa na
upungufu wa madawati 4,908.(Picha na Nathaniel Limu).
Kabelo
alitaja baadhi ya mikakati hiyo kuwa ni mfuko wa jimbo kutengeneza
madawati 345 yenye thamani ya shilingi 18,985,000 na fedha za mpango wa
lipa kwa matokeo (P4R) zitakazogharamia madawati 687 yenye thamani ya
zaidi ya shilingi 57.3 milioni.
“Aidha
kila kijiji kitagharamia utengenezaji wa madawati 25 (vijiji vipo 84
wilaya ya Singida),madiwani 29 wameahidi kuchangia madawati 58 yenye
thamani ya shilingi 3.1 milioni, mkurugenzi mtendaji wa halmashauri
Simion Mumbee atachangia madawati 6 yenye thamani ya shilingi
350,000.Wakuu wa idara na vitendo kila mmoja atachangia madawati mawili
na watumishji wa ofisi ya makao makuu,wamechangia shilingi 623
milioni”alisema.
Kwa mujibu wa mwalimu Kabelo,kabla ya harambee ya juzi,halmashauri ya wilaya ya Singida ilikuwa na uhaba wa madawati 4,908.
Post a Comment