Raphael Varane
Beki wa timu ya
taifa ya Ufaransa Raphael Varane ameachwa kwenye kikosi cha timu ya
taifa ya nchi hiyo.Varane hajajumuishwa kwenye kikosi kitachoshiriki
michuano ijayo ya Euro itayoanza mwezi June kutokana na kusumbuliwa na
majeraha ya nyama za paja.
Pia nyota huyu wa klabu ya soka ya Real
Madrid ataukosa mchezo wa fainali ya kombe la klabu bingwa ulaya
utapigwa Mei 28 kati ya timu yake na Atletico Madrid.Mchezaji huyu atakua nje ya uwanja kwa muda wa wiki tatu mpaka nne na nafasi yake kwenye kikosi cha taifa imechukuliwa na beki wa Adil Rami, mwenye umri wa miaka 30 anayeichezea timu ya Sevilla ya nchini Hispania.
Post a Comment