0
     
DODOMA
MBUNGE wa Liwale Zubeir Kuchauka ameishangaa serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kushindwa kujenga kituo cha polisi wilayani humo licha ya kuwa ina umri wa miaka 40.
Kuchauka alihoji swali hilo Bungeni jana wakati akichangia mada kwenye bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambapo alisema Wilaya hiyo ina kituo kimoja cha Polisi pia ni kibovu na kinafunikwa na maturubai wakati wa mvua kutokana na uchakavu wake.
Alisema waziri anatoa majibu mepesi yasiyoridhisha bila kuzingatia umuhimu uliopo katika kujenga kituo cha polisi kitakacholinda amani.
Alisema Waziri anazungumzia ujenzi katika vituo vingine 65 ambapo yeye mbunge afikirii kama katika wilaya hizo zitakua na umri mkubwa kama Liwale.
"Aliposema ni zaidi ya Wilaya 65 sidhani kama ina umri wa miaka 40 kama ilivyo Liwale ina jumla km 66.000 tarafa anazosema zipo zaidi km 60.kutoka Liwale mjini lakini hakuna kituo,"
"Hiko kituo ilichokuwepo mafaili yanafunikwa na turubai jengo linavuja na wamepanga kwenye nyumba ya mtu binafsi ya iliyokuwa  benki ya NBC sasa nahitaji nipewe majibu ni lini kituo kitajengwa.," aliongeza Kuchauka
Alisema hadi sasa kuna tarafa ambazo zimekua kibiashara zinahitaji kujengwa vituo kwa ajili ya ulinzi huku akivitaja kuwa ni pamoja Na Kibutuka,Lilombe,Miruwi,Makata na Mkutato kuna biashara ufuta na madini.
Awali Waziri Charles Kitwanga alisema hali ya uchumi ikiruhusu atafikiria kuwajengea kituo Liwale.

Post a Comment

 
Top