Harakati za vilabu vya Ulaya kuanza
kuwania saini za mastaa wanaowahitaji katika msimu wa 2016/2017
zimeshaanza, leo May 27 2016 stori kutoka The Mirror wameripoti klabu ya
FC Barcelona kufanikiwa kunasa saini ya kwanza katika dirisha hili la
usajili.
Barcelona wameripotiwa kutumia pound
milioni 2.8 kumsajili Davinson Sanchez kutoka klabu ya Atletico
Nacional, beki huyo kutoka Colombia atajiunga na FC Barcelona B lakini
atakuwa akifanya mazoezi na kikosi cha kwanza hiyo ni kwa mujibu wa
kocha wa FC Barcelona Luis Enrique.
Post a Comment