0

Aliyekuwa Kamishna Mkuu wa TRA Harry Kitilya na Bi.Shose Sinare,Siyoi Abraham Solomon wamefikishwa Na TAKUKURU katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kushtakiwa kwa makosa nane, ikiwemo utakatishaji fedha.
 
Aliyekuwa Kamishina Mkuu wa mamlaka ya mapato nchini TRA Harry Kitilya na wenzake wawili akiwemo aliyewahi kuwa miss Tanzania Bi Shose Sinare wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa  na mashtaka nane  likiwemo la kutakatisha fedha haramu.
Washtakiwa hao wamesomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Emilius Mchauru  ambapo Wakili Mkuu wa Serikali Oswald  Tibabyekomya amsema kati ya mashataka hayo nane Bi Sinare Kanaliwa ana mashtaka yote nane wakati wenzake wakabiliwa na mashtaka manne miongozi mwa mashtaka hayo.
 
 Inadiwa kuwa kati ya August 2012  na March 2013 katika jiji la Dar es Salaam washitkiwa hao wote kwa pamoja walikula njama ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu  kutoka katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Aidha watuhumiwa hao tarehe 5 Novemba 2012 katika Benki  ya  Stanbic makao  makuu yaliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam  walitengeneza mkataba wa kughushi  kuonyesha kuwa kampuni ya EGMA itaratibu upatikana wa mkopo wa dola za kimarekani milioni 550  kutoka Standard Bank ya London kwa kushirikiana  na Stanbic  ya Tanzania  na kisha wao wangejilipa asilimi 2.4 ya fedha hizo.
 
katika shtaka lingine watuhumiwa hao wote kwa pamoja  kati ya March 2013 na Septemba 2015 jijini dar es Salaam  walitakatisha fedha  dola za kimarekani milioni sita  kwa kuzihamisha kutoka katika  Account za  EGMA  zilizokuwa zimefunguliwa  Stanbic  Tanzania  kwa namba mbalimbali na kisha kuzihamishia katika akaunti za benki zingine  kama  KCB  wakijuwa kuwa fedha hizo hazikuwa safi badaa ya kusomewa mashtaka  hayo uliibuka mvutano wa kisheria kama wanaweza kupewa dhamana au laa hatua ambayo Hakimu anayendesha shauri hilo amesema atalitolea uamuzi ijumaa ijayo na hivyo washtakiwa  wamekwenda rumande.
 
katika kesi nyingine Mbunge wa Sumve Mh.Richard Ndasa amepandishwa katika kizimba cha mahakama hiyo mbele ya hakimu huyo  akikabiliwa na mashtaka mawili ikiwemo kujihusisha na vitendo vya rushwa ya shilingili milioni 30.
 

Post a Comment

 
Top