0
                       
Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makala, amebatilisha uuzwaji wa ardhi yenye ukubwa wa zaidi ya hekta 5000 zilizouzwa kwa wawekezaji na uongozi wa kijiji cha Luhanga wilayani Mbarali na kuamuru ardhi hiyo irejeshwe kwa wananchi, huku akiagiza watendaji wa serikali waliohusika na uuzwaji huo kuchukuliwa hatua.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Gabriel Makala akiwa kwenye mkutano wake wa kwanza na wanachi tangu ateuliwe kushika wadhifa huo, amechukua uamuzi mgumu wa kupokonya ardhi yenye ukubwa wa zaidi ya hekta 5000 kutoka kwa wawekezaji ambazo zinadaiwa kuuzwa na uongozi wa kijiji cha Luhanga na kuamuru ardhi hiyo ichukuliwe na wananchi.
 
Baada ya kutolewa kwa uamuzi huo, baadhi ya wananchi wamemshukuru mkuu huyo wa mkoa kwa madai kuwa uamuzi huo unahitimisha mgogoro uliodumu kwa miaka mingi kwenye kijiji chao.
 
Hata hivyo mkuu wa wilaya ya Mbarali, Gulamhussein Kifu akautaka uongozi wa kijiji hicho kuweka utaratibu mzuri wa kuigawa ardhi hiyo kwa wananchi, huku akiwaonya viongozi hao kujihusisha na vitendo vya rushwa wakati wa ugawaji wa ardhi hiyo kwa wananchi.
 

Post a Comment

 
Top