
Juma Abdul alizitoboa nyavu za APR kwa shuti kali kuiandikia Yanga bao la kwanza dakika ya 20 kwa mpira wa adhabu ndogo kufuatia Donald Ngoma kuangushwa na beki wa APR Rwatubyaye mita 10 kutoka kwenye box la penati.
Yanga itakuwa nyumbani kuikaribisha APR FC kwenye mchezo wa marudiano utakaochezwa March 19, 2016 kwenye uwanja wa taifa, Dar es Salaam.
Takwimu muhimu
- Yanga imekutana na APR FC kwa mara ya tatu kwenye michuano ya klabu bingwa barani Afrika. Mchezo wa kwanza kuzikutanisha timu hizo, Yanga ilikubali kichapo cha bao 1-0 lakini leo Yanga imeshinda kwa bao 2-1.
- Haruna Niyonzima na Mbuyu Twite walikuwa wanacheza dhidi ya timu yao waliyowahi kuitumikia miaka kadhaa iliyopita.
- Kikosi cha APR kilichocheza dhidi ya Yanga kilikuwa na wachezaji wazawa kwa 100% wakati Yanga walikuwa na wachezaji mchanganyiko, wachezaji wazawa na wale wa kigeni.
Post a Comment