0

Wabunge wamevitaka vyombo vya kuichunguzi kuhakikisha vinazifanyia kazi tuhuma  za rushwa zinazowakabili baadhi ya wabunge kwani ni dhahiri zinashusha hadhi ya Bunge na kuwafanya wananchi kutokuwa na imani na wawakilishi wao.
Katika mahojiano maalum na ITV kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam wabunge hao kutoka majimbo ya Mtera,Nyamagana,Magomeni Visiwani Zanzibar wamesema uwepo wa tuhuma hizo kwa wabunge waliopewa dhamana kubwa ni fedheha kwa Bunge, huku wakitaka hatua stahiki kuchukuliwa kama tuhuma hizo zitabainika.
 
Maafisa wa Bunge wanasema moja ya hatua za awali waliokwisha kuzichukua ni pamoja na kuwavua uwenyeviti wa kamati za kudumu za bunge wanaotajwa katika tuhuma hizo pamoja na kuwahamisha baadhi ya wabunge kutoka kamati moja hadi nyingine,nakuahidi hatua nyingine zaidi zitafuata.
 
Miongoni mwa hatua zilizokwisha kuchukuliwa na Spika wa Bunge chini ya kanuni ya  116(3) cha kanuni za kudumu za Bunge,ni pamoja na kufanya mabadiliko katika kamati 5 za Bunge pamoja na kufanya mabadiliko ya wajumbe katika kamati hizo.

Post a Comment

 
Top