
Waziri
wa Kilimo Mifugo na Uvuvi Mh. Mwigulu Nchemba akifafanua jambo wakati
wa mazungumzo yake na Balozi wa Ubelgiji nchini Bwana Paul Cartier na kulia kwa Balozi ni Afisa kutoka Ubalozi huo Bibi. Isabelle Wittoek
(Picha Maktaba)
Na.Ahmad Mmow,Lindi.
Imeelezwa
kwamba, japokuwa sekta ya kilimo nchini inatoa 95% ya mahitaji ya
chakula, na kuchangia 30% ya mauzo ya nje. Lakini bado mfumo wa masoko
uliopo unachangamoto kubwa.
Hayo
yalielezwa jana mjini Lindi, na meneja mahusiano wa mamlaka ya masoko,
dhamana na mitaji, Charles Shirima, wakati wa mafunzo ya uanzishwaji wa
soko la bidhaa, ikiwamo za kilimo.
Shirima
ambae alikuwa ni miongoni mwa watoa mada katika mafunzo hayo, alisema
pamoja na juhudi za kuboresha mfumo wa masoko zinazofanywa na serikali,
bado kunachangamoto kubwa.
Kwasababu
mfumo uliopo haujakidhi ipasavyo mahitaji ya masoko ya mazao ya kilimo.
Meneja huyo alisema mfumo wa soko bado umehodhiwa na wanunuzi wachache
ambao wamekuwa wakipanga bei za kununulia mazao, hivyo kusababisha
kukosekana ushindani.
Alisema
mfumo wa masoko uliopo hautabiriki na matatizo mengi, ikiwemo wanunuzi
kufanya migomo ya kununua mazao ya wakulima wakati serikali
inapoingilia kati kwa kutoa bei elekezi ili kuwasaidia wakulima
wasidhulumiwe.
"Vilevile
taarifa za masoko, hususani bei na kiasi kilichouzwa na kununuliwa
bidhaa zilizopo sokoni zimekuwa hazitolewi kwa wakati na uwazi kwa
wakulima wote," alisema Shirima.
Kwa
upande wake, katibu tawala wa mkoa wa Lindi, Ramadhani Kaswa, elimu
kuhusu masoko haina budi kufikishwa kwa wakulima wa vijijini, ili
kuwanusuru wasinyanyaswe na kupunjwa na wajanja wachache ambao hawavuji
jasho kama wakulima hao.
Pia
alitoa wito kwa vyama vikuu vya ushirika vilivyopo katika mkoa huu
kuyatambua mazao mengine ya kilimo yanayolimwa katika mkoa huu, badala
ya kutegemea korosho na ufuta pekee.
Nae
meya wa manispaa ya Lindi, Mohamed Liumbo, alisema pamoja na mfumo
mzuri wa stakabadhi za mazao ghalani, lakini wakulima wanakero nyingi. Hivyo kunahaja ya viongozi na watendaji kuepuka kasoro zinazotokana na uzembe.
Post a Comment