wananchi wakiwa kwenye mkutano wakisikiliza kwa umakini mambo muhimu kutoka kwa viongozi mbalimbali
wananchi wakiwa kwenye mkutano wakisikiliza kwa umakini mambo muhimu kutoka kwa viongozi mbalimbali
Mbunge wa jimbo la Liwale mh.Zuberi Kuchauka akiongea na wananchi na kuchukua kero mbalimbali ili kuweza kupeleka bungeni
NA Mwandae
Mchungulike,Liwale
Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Liwale bwana Mohamedi
Mtesa amewashukuru wanachi kwa kuweza kuwachagua viongozi makini watakao weza
kufanya kazi za kimaendeleo walizotumwa na wananchi.
Hayo aliyasema jana kwenye mkutano ulifanyika katika kata ya
Nangando tarafa ya Liwale mjini mkoani Lindi.
“Ndugu
zangu mumetupa kazi tatu za kufanya na sisi kazi za kufanya tunazijua kazi ya
kwanza kutetea haki zenu,kusimamia uwepo wa maendeleo katika halmashauri yetu na
kuhakikisha usalama wa wananchi tumeanza nayo na tunayafanyia kazi pia napenda
kuwaambia kuwa mchango wa kukatwa shilingi 30 kwa kilo za mazao sasa umefutwa tunajua sisi Halmashauri tunaumia ila kwakuwa mulikatwa
kwa muda mrefu sasa tunabalansi”alisema Mtesa.
Mtesa alisema maliasili imekuwa mwiba kwa wananchi wa wilaya ya Liwale
amewaomba kwa nia njema kama viongozi wa halmashauri jukumu la maliasili ni
kulinda wanyama lakini pia wanahitaji ushirikiano wa ulinzi kutoka kwa wananchi
lakini hawawezi kufanya kazi ya ufanisi bila ushirikiano wa wananchi.
Alisema mazao ya wakulima yanaliwa na Nguruwe ikitokea
Nguruwe ameuwawa wananchi wanachukuliwa hatua kali ambayo haiendani na
kosa pia amewashauri maliasili
wanatakiwa kuwa na busara kwa wananchi ili kuweza kupata ushirikiano na
wananchi.
“Hatuhalalishi ujangili kama kuna mtu anashughulika na
ujangili tunamuomba aache sisi hatutawatetei ujangili sisi tunahitaji kujenga
ila tunahitaji bao za milango kama jambo hili halitakuwa na mabadiliko
hatawaunga mkono lakini yakitokea mabadiliko mazuri nitaungana nao kupita
kijiji hadi kijiji kuwahamasisha wananchi kuwapa elimu sasa tunasubiri matokeo
kama yatakuwa siyo na sisi tutasema siyo”alisema Mtesa.
Mtesa alisema watu wafanye kazi kwa bidii ili watu
wajiongezee kipato jambo kubwa la kufanya kazi kwa kujituma halmashauri imekuja
na mkakati wa kuwahamasisha wananchi kuongeza zao mbadala la biashara la
arizeti kwani ardhi ya Liwale inastawi mahali popote hatuwezi kuendelea
kutegemea mazao ya korosho na ufuta tu lazima tuongeze zao jingine ili kipato
kiongezeke.
Tatizo la viwanja watu
wamepewa viwanja lakini watu wamekaa kimya hawajavilipia mpaka sasa Mtesa
alibainisha kuwa kama wananchi waliopewa viwanja inakuwa tatizo kulipia kwa wakati ,walipopewa
viwanja waliambiwa baada ya siku 21 wawe wametanguliza kutoa shilingi laki
mmoja (100,000/=) kwa kiasi cha thamani ya kiwanja alichopewa lakini watu wameshindwa
kulipia hata shilingi toka septemba
mwaka 2015 watu wa aina hii hawatavumiliwa kwani watu wengine wanahitaji
viwanja pia ili kuweza kumaliza tatizo
la viwanja kwa watu wanaodai toka mwaka 2009.
Kwa upande wake mbunge wa Liwale Mh.Zuberi Kuchauka alianza kwa kuwashukuru wananchi wakati
anaomba ridhaa kwa kupita kila kijiji aliwahaidi wananchi kuwa yeye atakuwa
sauti kwa waliokosa sauti na atakuwa mwakilishi kwa waliokosa mwakilishi na kusema kuwa kwa sasa muda wa
kufanya siasa umekwisha bali yeye ni mbunge wa Jamhuri ya muungano wa
Tanzania na si mbunge wa chama kimoja au watu wachache huku akisema kuwa yeye ni mpenda maendeleo
hivyo kwa kushirikiana na wananchi walioko katika jimbo lake washirikiane kwa
pamoja kufanya kazi kama sera ya muheshimiwa rais Magufuli inayosema [ hapa
kazi tu].
Pia mheshimiwa Kuchauka akabainisha kuwa mara baada ya
kuapishwa kuwa mbunge akaanza na dhiara
mbalimbali ikiwemo kutembelea katika sekta mbali mbali ikiwemo Mashirika ya umma ,mashirika binafsi,na ikiwemo idara
ya Kilimo ,Afya ,maliasili,maji Mahakama ,Polisi, huku akisema kuwa AFYA;kwa
upande wa sekta ya afya bado huduma si mzuri na
hospitali ya wilaya ya Liwale haina hadhi ya kuitwa hospitali pia anahitaji
kuepo kwa dhahanati kila kijiji hivyo amedai kuwa atapambana na hali
hiyo huku akiweka kipaumbele kikubwa katika afya kwakuwa afya ndio kila kitu
katika jamii na kuhaidi kutekeleza uwepo wa huduma mzuri kwa wakinamama
wajawazito na watoto huku akisema amepeleka kapeti za kutosha pamoja na gloves
huku akihaidi kupeleka ndoo na mabesen kwa ajili ya akinamama wajawazito.
Huku akisema kuwa
amefanya jitihada za kurekebisha mashine ya x-ray na sasa inafanya kazi
pia amewaomba wana Liwale wajiunge na
mfuko wa bima ya afya wa CHF ambao
utawawezesha kupata matibabu kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa shilingi alfu kumi
kwa watu 6 kwa kila kaya na kusema yeye ameweza kuchangia kaya 100 na tayari
amesha lipia kiasi cha shilingi million 1 huku akitoa changamoto ya watu kutopata dawa mara baada
ya matibabu hivyo amewataka wahusika kuwa makini katika huduma hiyo muhimu.
ELIMU;Mara baada ya kuhitimisha katika sekta afya mheshimiwa aliongelea pia katika sekta ya
Elimu na kusema kuwa bado hali ya ufaulu kwa shule za sekonali wilaya ya Liwale
si mzuri huku akisema shule ya sekondari
liwale day tu ndiyo angalaau imeweza kutoa division 1 tano tu kwa willaya mzima hivyo
amewataka wazazi washirikiane na walimu katika kuhakikisha maendeleo ya
wanafunzi yaweze kuwa mazuri pia amezungumzia upande wa elimu yamsingi na
kusema kuwa kuna uhaba mkubwa wa walimu ,uhaba wa madarasa ,nyumba za walimu
huku akiwataka wazazi wanaohamahama kwenda mashambani wahakikishe sehemu
wanazohishi zinapatikana huduma zote za jamii ili kurahisisha watoto wao kupata
elimu.
KILIMO;Pia katika sekta ya kilimo ameweza kubainisha
changamoto kwa kusema kuwa watu wengi wamejisahau badala ya kulima mazao ya
chakula wengi hulima mazao ya biashara
na kusema kuwa changamoto nyingine ni kuwa
maafisa ugani ni mizigo kwa baadhi
ya maeneo ya vijijini kama Mpigamiti,kikukulyungu na mirui ambayo huchangia wakulima kushindwa kufanya
vizuri katika kilimo kwakuwa maafisa wengi wanakaa tu maofisini bila
kuwatembelea wakulima huku akisema kuwa changamoto nyingine ni uwepo wa nguruwe
ambao wanamaliza mazao na kusema kuwa ameshaenda maliasili mara tatu nakumtaka
mkuu wa kitengo cha maliasilia atumie hekima ambayo itaweza kutatua tatizo hili
na si kwa kuwapa fain kubwa wakulima
wanaoua nguruwe huku wanyama hao wanama liza mazao.
MGOGORO WA MPAKA;Kijiji cha kikulyungu na selous amesema
shughuli za utalii zisimame kwa sababu eneo lile lina mgogoro lakini pia
alizungumzia mgodi uliyoko lilombe na kukuta hakuna unufaikaji wowote kwa wanakijiji ama halmashauli
kutokana na uchimbaji unaoendelea katika eneo hilo bali wanaochimba katika eneo
hilo huwa wanalipia nachingwea na kupata kibali huko hivyo hakuna manufaa
yoyote kitika mgodi huo hiyo mheshimiwa mbunge amehaidi kufwatilia swala hilo
ili kuhakikisha manufaa yanapatikana.
POLISI;mheshimiwa pia amebainisha ukosefu wa vituo vya polisi
katika maeneo ambayo yanakuwa kimaendeleo na kibiashara katika wilaya ya liwale
kama vile kijiji cha Kibutuka na Lilombe
na kuhaidi kujitahidi kufwatilia na kuhakikisha maeneo hayo nayo yanakuwa na
vituo.
MAJI;Pia ametembelea maeneo mbalimbali ambayo yanachangamoto
za maji na kusema kuwa tayari serikali ilikwisha toa million miambili ambazo ni
za miundombinu ya maji wilayani liwale.
Pia akazungumzia swala
la mahindi ambayo baadhi ya watu
wanamshutumu kuwa amemuuzia mahindi ambayo ni msaada wa wananchi liwale
mfanyabiashara aliyoko wilayani hapo Bwana Amidu Wamo si sahihi na awezi
kufanya kitu kama hicho bali kama mahindi ya serikali ambayo yanauzwa shilingi
150 kwa kilo hayo yamefikia katika halmashauri ya wilaya ya liwale na madiwani
wote wanafahamu.




Post a Comment