0

Tanzania - Kilwa
 
Na. Ahmad Mmow, Kilwa.

Watalamu wa Afya Wilayani Kilwa wametakiwa kuzingatia maadili ya taaluma yao na utumishi wa umma wanapotekeleza majukumu yao.
 
Njwayo alisema hayo jana alipozungumza na wananchi katika kijiji cha Miteja baada ya kuweka jiwe la msingi nyumba mganga wa zahanati ya kijiji hicho, iliyojengwa kupitia mfuko wa Rais wa maendeleo ya jamii(TASAF). 

Alisema miongoni mwa mambo yanayosababisha malalamiko kwa wananchi ni baadhi ya watumishi wa umma ikiwamo wa idara ya afya kufanya kazi kwa mazoea kwakutozingatia maadili ya taaluma zao na utumishi wa umma.

Huku baadhi yao wakikosa uadilifu kwa kuiba mali na vifaa vya umma, ikiwamo dawa kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali.
"Baadhi ya wakunga mnakiuka maadili ya taaluma yenu na kusababisha akina mama wajawazito kuona afadhali wakati wakujifungua wasaidiwe na wauguzi wa kiume, kutokana na lugha chafu mnazowatolea", alisema Njwayo.

Mkuu huyo wa Wilaya ambae anakaribia kutimiza miezi sita tangu ateuliwe kushika wadhifa huo na kuhamia katika wilaya hii,aliongeza kusema licha ya kukiuka maadili lakini pia wapo ambao siowaaminifu.
"Haiwezekani dawa ziletwe leo, na kesho ziwezimekwisha. Gari iliyoleta ikiondoka tu, na dawa zinakwisha" Waliosoma wapo wengi lakini hawana kazi, kama hamtaki kuzingatia maadili basi ondokeni," alisisitiza.

Aidha alizitaka kamati na bodi za afya kufuatilia kwa karibu matumizi ya dawa zinazopelekwa katika maeneo yao ili kuisaidia serikali kudhibiti wizi. Mkuu huyo wa Wilaya licha ya kuweka jiwe la msingi jengo hilo ambalo ujenzi wake umegharimu shilingi 68.06 milioni, lakini pia alizilipa ruzuku kaya maskini 176 zilizopo katika kijiji hicho. Ikiwa ni awamu ya tatu ya utekelezaji wa mpango huo yanayofanywa na TASAF katika wilaya hii.

Kwa upande wake diwani wa kata ya Miteja, Ibrahimu Msati, aliiomba serikali kumpeleka mganga katika zahanati hiyo ambayo pia inawahudumia wananchi wa vijiji jirani vitatu. 

Huku akitoa wito kuzipa kipaumbele zahanati zilizo mbali na hospitali kwa kuzipelekea haraka dawa,vifaatiba na wataalamu.

Post a Comment

 
Top