0
Leo katika ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa katika kituo cha Liwale kulikuwa na mchezo mkali kati ya Mikukuyumbu world soccer Vs Stand Worriers mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa wilaya ya Liwale.

 Kwa kipindi cha kwanza kila timu ikianza kwa mbwembwe ikitafuta bao mapema lakini bahati ilikuwa kwa timu ya mikukuyumbu katika kipindi cha kwanza hiko iliongoza kwa kupachika  bao 2 mabazo ziliofungwa na mchezaji mmoja  Huseni Mchite namo dakika ya 36 na dakika ya 41 kipindi cha kwanza.

Katika kipindi cha pili stand worriers kutoka mkoani Lindi waliweza kupata bao moja lililofungwa na Halfani Musa namo dakika ya 90 Mpaka mchezo unamalizika matokeo yalikuwa Mikukuyumbu world soccer 2-1 Stand worriers

Post a Comment

 
Top