kwa upande wa kushoto ni Mratibu wa CHF wilayani Liwale bwana Evarist Malima alikaa katikati Mary Ding’ohi afisa maendeleo ya
jamii na Brigton Makelele mwakilishi wa Wama wilayani Liwale.
Katibu tawala wilaya ya Liwale mkoani Lindi Wilson Nyamanga aitisha kikao
leo ofisni kwake kilichohusisha Taasisi mbalimbali na waandishi wa habari kwa
lengo la kutafuta utatuzi wa changamoto zilizopo katika jamii.
Akizungumza na Taasasi zisizo za kiserikali ya OlidIngo,viongozi
wa vikundi vya vikoba na mratibu wa bima ya afya ya jamii CHF alisema azima ya
kuitisha kikao hicho ni kutaka viongozi wa vikundi kuwahamasisha wanachama wao
wote wa vikoba vilivyopo hapa wilayani
kuweza kujiunga na mfuko wa bima ya afya ya jamii ambayo huchangia kiasi cha
shilingi 10000 hutibiwa kaya moja yenye
watu 6 na kuifanya kaya hiyo kuweza kutibiwa kipindi cha mwaka mzima.
Kwa upande wake Brigton Makelele mwakilishi wa Wama wilayani Liwale
alisema amefurahishwa sana kikao hicho na kufungua ukurasa mpya wa mahusiano
pia amebainisha kuwa kunauwezekano mkubwa sasa wa kutembelea vikundi mbalimbali
vilivyopo hapa wilayani na kuwahamasisha kuweza kujiunga na mfuko wa bima ya
afya ya jamii kupitia pesa wanazochangishana katika vikundi hivyo ambazo huitwa
pesa za tahadhari na kuweza sasa kujiunga na mfuko wa bima ya afya ya jamii kwa
lengo la kujihakikishia kuweza kupata matibabu ya mwaka mzima.
Mratibu wa CHF wilayani Liwale bwana Evarist Malima alisema
kila Mtanzania ni vyema akajiunga na bima ya afya kwa kuzingatia kwamba bima
hii hakuna masharti magumu katika kujiunga kwake pia ameziomba Asasi mbalimbali
kuweza kusaidia kuzilipia kaya zisizojiweza au maskini katika maeneo yao
aliongeza kusema hadi sasa watoto wanaoishi katika mazingira magumu wameweza
kuwaunganisha kwenye mfuko huo ni 1260.
Viongozi wengine waliohudhulia kwenye kikao hicho ni Mary Ding’ohi afisa maendeleo ya
jamii alisema idara yake inafanya kazi
na Taasisi mbalimbali zilizilizopo hapa wilaya na kufuatilia kwa ukaribu katika
vikundi vyote na popote vilipo bila kuangalia kipo chini ya nani.
Katibu wa Olidingo
ambayo ni NGO’S bwana Ally Ligai alisema
Olidingo ni mratibu wa washughuli zote za vikundi hapa wilayani Liwale na kufanyakazi
ya pamoja kwa kufuata kanuni na utaratibu pia alibainisha kuwepo kwa changamoto
ya ushirikiano mdogo kwa baadhi ya Taasisi zinazokuja kufanya kazi hapa
wilayani bila kushirikiana na Olidingo na kusababisha jamii kukosa kupata
taarifa sahihi na aliongeza kusema kupitia kikao hichi wamefungua ukurasa mpya
wa ushirikiano katika utendaji kazi.
Katibu tawala akifunga kikao alibainisha kuwa kwa jitihada za
viongozi wa serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wameweza kushawishi
kaya zaidi kutoka 2110 na kuongezeka baada ya kufanya kampeni ya kuwashawishi
wananchi hadi sasa idadi ya kaya zimeongezeka na kufikia kaya sasa zaidi ya
5000 na wanatarajia kupata ongezeko kubwa zaidi ya hapo, idadi kamili itaelezwa
katika kikao cha tathumini kinachotarajia kufanyika mwezi march 2 mwaka huu pia
aliongeza kusema serikali kwa
kushirikiana na Taasasi mbalimbali kupitia kikao hiki wameadhimia kuitisha
mkutano mkubwa uliopewa jina la jukwaa
la wadau wa Liwale.


Post a Comment