0
 Salva
Salva Kiir ameomba msamaha akifungua mkutano mkuu wa SPLM
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir kwa mara ya kwanza amewaomba radhi raia wa nchi hiyo kutokana na mateso na dhiki ambayo wamepitia wakati wa mzozo wa kisiasa uliodumu miaka miwili.
Bw Kiir amesema kuomba msamaha ndiyo hatua ya kwanza katika kufanikisha maridhiano nchini humo.
Amechukua hatua hiyo wakati wa kufungua rasmi mkutano mkuu wa chama tawala cha SPLM.
Kutoelewana katika mkutano sawa mwaka 2013 kulitangulia jariibo la mapinduzi ya serikali nchini humo na mapigano yaliyodumu miezi mingi.
Mkataba wa Amani ulitiwa saini mwezi Agosti mwaka jana mjini Addis Ababa, ingawa Rais Kiir alitia saini mkataba huo shingo upande.
Jana, pande zilizohusika katika mzozo huo ziliafikiana kuhusu kugawana nyadhifa za uwaziri katika baraza la mawaziri la serikali ya umoja.
“Hebu niwaambie, wenzangu, kwamba mimi, kama Mkristo, imenibidi kujitafakari jambo ambalo ni hatua kuu kwetu sote kama taifa moja na kufikia uwiano na umoja,” alisema Bw Kiir.

Post a Comment

 
Top