Uongozi wa klabu ya Real Madrid hatimaye umemfukuza kocha wake Rafael Benitez ambaye amedumu kwa miezi 7 pekee.
Nafasi ya Benitez imechukuliwa na aliyekuwa mchezaji wa Ufaransa
Zinedine Zidane ambaye awali alikuwa kocha wa kikosi B cha Real Madrid.
Tangu atue Madrid, Benitez amekuwa hapendwi na mashabiki wa klabu hiyo, baada ya kufungwa bao 4-0 kwenye mechi ya El Clasico mwezi Novemba na mahasimu wao Barcelona, pia kutupwa nje ya michuano ya Copa del Rey.
Post a Comment