0

Tokeo la picha la ONLINE

Bofya hapa kwa habari za karibuni zaidi
19:56 MECHI ZINAMALIZIKA
  • West Ham 2-0 Liverpool
  • Arsenal 1 -0 Newcastle
  • Leicester 0-0 Bournemouth
  • Man Utd 2-1 Swansea
  • Norwich 1 -0 Southampton
  • Sunderland 3-1 Aston Villa
  • West Brom 2-1 Stoke
19:53 Manchester United 2-1 Swansea
David de Gea anafanya kazi ya ziada kumzuia Ashley Williams kufunga.
19:51 Sunderland 3-1 Aston Villa
Jermain Defoe anafungia Sunderland bao la tatu.
19:50 West Brom 2-1 Stoke
Jonny Evans anafungia West Brom bao, ambao huenda likawahakikishia ushindi. Ni dakika ya 93. Hilo ndilo bao lake la kwanza tangu 2012.
19:48 Arsenal 1-0 Newcastle
Sekunde chache baadaye, Mesut Ozil anatikisa wavu, lakini kutoka upande wa nje.
19:47 Arsenal 1-0 Newcastle
Aaron Ramsey anapoteza nafasi nzuri ya kufunga. Mpira wake unatoka nje.
19:45 West Brom 1-1 Stoke
Geoff Cameron wa Stoke anaonyeshwa kadi nyekundu.

19:38 Baooo! West Brom 1-1 Stoke
Huko Hawthorns, Jon Walters anasawazishia Stoke City.
19:35 Baooooo! Manchester United 2-1 Swansea
Wayne Rooney anafungia Man Utd la pili dakika ya 75 baada ya kupokea pasi kutoka kwa Anthony Martial .
19:33 Baoooo! Norwich 1-0 Southampton
Alexander Tettey anafungia Norwich dakika ya 74.
19:32 Sunderland 2-1 Aston Villa
Jermain Defoe anarejesha Sunderland mbele.
19:30 Norwich 0-0 Southampton
Mkenya Victor Wanyama anapewa kadi nyekundu.
19:29 Baooo!Arsenal 1-0 Newcastle
Laurent Koscielny anaweka Arsenal kifua mbele.
19:29 Baooooo! Manchester United 1-1 Swansea
Gylfi Sigurdsson anasawazishia Swansea.
19:22 Manchester United 0-0 Swansea
Andre Ayew anapata nafasi. Anajipenyeza kati ya walinzi wawili wa Man Utd lakini mpira wake wa kichwa unagonga mlingoti wa goli.
19:20 Baoooo! Sunderland 1-1 Aston Villa
Carles Gil anasawazishia Aston Villa.
19:17 Baooo!West Brom 1-0 Norwich
Stephane Sessegnon anafungia West Brom.
19:15 Leicester 0-0 Bournemouth
Riyad Mahrez anashindwa kufunga penalti.
19:14 Leicester 0-0 Bournemouth
Leicester wanapata penalti na Simon Francis wa Bournemouth anaonyeshwa kadi nyekundu kwa kumwangusha Jamie Vardy.
19:09 Leicester 0-0 Bournemouth
Leicester wanapoteza nafasi nzuri sana ya kufunga.
Jamie Vardy anatoa kombora lakini linatemwa nje. Kona inapigwa lakini mpira wa Wes Morgan unapaa juu ya wavu.
19:07 BAOOO! Manchester United 1-0 Swansea
Anthony Martial anafungia Man Utd kwa kichwa.

Post a Comment

 
Top