0

Wananchi katika kijiji cha Kaswa kata ya Miswaki wilayani Uyui mkoani Tabora, wameiomba serikali kuwasaidia kuimarisha barabara na daraja la Kaswa ambalo limekuwa kiunganishi cha kwenda katika hospitali ya rufaa ya Nkinga kupata huduma za afya zikiwemo za upasuaji.
Wakizungumza na ITV katika daraja hilo ambalo linaonyesha kutoimarishwa kiujenzi wananchi hao wamesema kuwa, kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha wilayani humo, zinaweza kuliondoa kabisa na matokeo yake ni kusababisha madhara makubwa yakiwemo ya vifo vya wagonjwa. 
 
Akizungumzia daraja hili diwani wa kata hiyo Bw, Anthony Simon  Makani amesema kuwa, wananchi wanategemea huduma mbalimbali za kijamii kupitia daraja hilo, hivyo serikali ingewaangalia kimsaada zaidi ili kuliimarisha kwa lengo la kuwanusuru na majanga ambayo yanaweza kusababishwa na daraja hilo.

Post a Comment

 
Top