Papa Francis, atatoa ujumbe wa Krismasi kwa waumini baadaye leo
Papa alikuwa akiongoza maadhimisho ya mkesha wa Krismasi katika mida ya St Peter's Basilica mbele ya waumini takriban 10,000.
Baadaye leo Ijumaa, atatoa ujumbe wa kila mwaka wa Krismasi kutoka kwenye roshani ya mida ya kanisa hilo la St Peter's.
Alipokuwa akiongoza ibada ya misa, Papa alisema Krismasi ni wakati mwingine wa kujitambua na kujitafakari.
Aliwahimiza waumini kuonyesha maisha ya ukawaida kama alivyofanya mtoto Yesu, “alipozaliwa katika maisha ya ufukara katika zizi la ng’ombe licha ya utukufu wake” kama mwongozo katika maisha yao.
“Katika jamii hii ambayo kawaida imeleweshwa na mtindo wa kutumia mali kwa wingi, anasa na utajiri, mtoto huyu anatuhimiza tufanye mambo kwa kiasi, kwa njia ambayo ni rahisi, ya kufanya mambo kwa kipimo, na kufanya mambo yaliyo ya muhimu,” alisema.
Usalama uliimarishwa wakati wa ibada hiyo na polisi walikuwa wakipekua watu na magari maeneo yaliyo karibu na Vatican.
Wote walioingia kwenye kanisa hilo, ambalo ndilo kubwa zaidi duniani, walilamika kupitia kwenye mitambo ya kupekuwa watu kutambua vyuma.
Waandishi wa habari wanasema Papa Francis, 79, alitumia mahubiri hayo kuangazia mada kuu ambazo ameangazia katika uongozi wake – msamaha, huruma, kuhisi hisia za watu wengine na kutenda haki.
Sauti yake ilikuwa hafifu wakati mwingine, kutokana na mafua yaliyokuwa yamempata mapema wiki hii.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.