Taifa la Burundi limelishtumu taifa jirani la Rwanda kwa kuwafunza waasi wanaotaka Kuvuruga hali ya usalama nchini humo.
Taifa
hilo limesema kuwa Rwanda inamhifadhi kiongozi wa jaribio la mapinduzi
yaliotibuka mbali na kuwasaidia waasi kutekeleza mashambulizi
mipakani,waziri wa maswala ya kigeni Alain Nyamitwe ameiambia BBC.Rwanda imekana madai hayo na kusema Burundi inajaribu kupotosha watu kuhusu matatizo yake.
Nkurunziza
Serikali hizo mbili zina uhusiano uliojaa hofu ,huku mataifa yote yakiwa na makabila yanayofanana.
Burundi imekumbwa na mauaji kadhaa pamoja majaribo ya mauaji tangu rais Pierre Nkurunziza ashinde uchaguzi uliokumbwa na utata mnamo mwezi Julai.
Post a Comment