Mechi
ya kirafiki baina ya Mbeya City FC dhidi ya mabingwa wa kabumbu
Tanzania bara, Dar es salaam Young Africans tayari imeanza kuteka hisia
za mashabiki wa soka jijini Mbeya.
Mchezo huo utakaopigwa Jumapili ya wiki hii uwanja wa sokoine Mbeya utaanza majira ya saa 10:00 jioni.
Wenyeji wa mtanange huo wametangaza kiingilio kuwa ni Shilingi 40,00/=
Mbeya City haijawahi kuifunga Yanga katika mechi mbili walizokutana uwanja wa Sokoine.
Msimu wa mwaka juzi, City wakiwa katika ubora wa hali ya juu walitoka sare ya 1-1 dhidi ya Yanga na msimu uliopita walikufa 3-1.
Uwanja
wa Taifa Dar es salaam, pia Mbeya City haijawahi kuifunga Yanga kwani
mechi ya kwanza msimu wa 2013/2014, Wanajangwani walishinda 1-0 na msimu
uliopita walikinyuka 3-1 kikosi hicho cha Juma Mwambusi .
Kwa maana hiyo, Yanga imeshindikana mbele ya Wagonga nyundo wa Mbeya.
Je, watapindu rekodi hii Jumapili?

Post a Comment