0



KOCHA bora wa msimu wa 2014-15, Mbwana Makata, amesema tuzo aliyopewa juzi na mdhamini wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Kampuni ya Vodacom ameitoa kama zawadi kwa mke wake, Mwangaza Makata kwa kumpa sapoti kwenye vipindi vigumu alivyopitia wakati akifundisha soka.
Makata juzi amewashinda Mserbia, Goran Kopunovic aliyekuwa Simba SC na Mholanzi Hans Van Der Pluijm wa Yanga katika tuzo ya kocha bora, baada ya kuinusuru Prisons kushuka daraja.
Kutokana na kutwaa tuzo hiyo, kocha huyo alizawadiwa kitita cha Sh milioni 8.6.
Akizungumza na Mtandao huu leo
, Makata alisema tuzo aliyopewa anaitoa kama zawadi kwa mke wake huyo hasa kutokana na uvumilivu alionao kwake wakati wote ambao amekuwa akifundisha soka.
“Nina furaha ya ajabu, kifupi nimestahili kuwa kocha bora msimu huu kwakuwa  Prisons niliikuta katika mazingira mabovu sana.
‘Kwa kutambua hilo, tuzo hii naitoa kwa mke wangu, wachezaji na viongozi wa Prisons kwa kuweza kupambana na kuibakisha timu ligi kuu.
“Mimi ni daktari katika soka, hivyo lazima niwatibu wagonjwa, wakati naichukua Prisons kila mtu aliniona kama mpenda pesa tu, kumbe sio hivyo, nilikaa nao chini na kuwapa mbinu za kuweza kupata ushindi na tumefanikiwa,” alisema Makata.
Makata anatarajia kutua Kagera Sugar kuchukua mikoba ya Mganda Jackson Mayanja ambaye uongozi wa klabu hiyo ulimfungashia virago baada ya msimu uliopita kufikia tamati.




Post a Comment

 
Top