0


Mwaandishi wetu Kilwa
Wananchi wa kata ya Mitole wilayani Kilwa mkoani Lindi wameiomba serikali chakula cha msaada ili  kukabiliana baa la njaa linalowakabili lilosababisha  na ukosefu wa mvua.
Ombi hilo liletolewa na wananchi hao wakati walipokuwa wanazungumza  na timu ya waandishi wa habari waliotembelea kijiji hapo.    
Akizungumza kwa niaba ya wakazi wa kijiji hicho Haji Katumbusi alisema wananchi  wameanza kwenda porini kutafuta matunda na mizizi (Angadi)kwa ajili ya chakula ili kukabiliana  na hali hiyo.
Katumbusi alisema kuwa katika kijiji chao kuna hali mbaya ya ukosefu wa chakula jambo ambalo uwalazimu kwenda kutafuta matunda na  mizizi ya porini ili kujikimu.
“Hali kwa kweli ni mbaya kwani wananchi  wanatumia muda mwingi na kutembea umbali mrefu kutafuta matunda ya pori, mizizi ili iweze kuokoa maisha ya watoto  baada ya kutumika kama chakula” alisema Katumbusi
Nae Diwani wa kata ya Mitole wilayani Kilwa Rafii Kuchao alikiri kuwepo kwa tatizo  hilo la njaa na kuiomba serikali kupeleka chakula cha bei nafuu  haraka na cha  kutosha  ili kiweze kuokoa maisha ya wananchi wa kata hiyo.
“Wanawake na watoto ndiyo wanaodhirika sana  na tatizo ili la njaa kutokana na kundi hili kutoweza kukimbia kutoka nje ya kijiji na maeneo menginen kwa lengo la kujisalimisha” alisema Kuchao
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya Kilwa Abdala Ulega alisema tayari ofisi yake imetoa taarifa  kwa mkuu wa mkoa Lindi  na limefanyiwa kazi  kwani mpaka sasa   tani 200 za mahindi zimeshafika ambazo zitapelekwa maeneo na vijiji 84  wilayani humo  vilivyokubwa  na  tatizo la njaa

Post a Comment

 
Top