0
   Mkuu wa wilaya ya Liwale mheshimiwa Ephraim Mmbaga
Mkuu wa wilaya ya Liwale mheshimiwa Ephraim Mmbaga mkoani Lindi amesema serikali ya wilayani hapa kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wameandaa hafla maalumu ya walemavu wilayani Liwale.
  Mkuu wa wilaya aliyasema hayo jana kupitia ukurasa wake wa facebook hafla hiyo maalumu itafanyika siku ya jumapili tarehe 29/3/2015 katika ukumbi wa Tengeneza Liwale kuanzia majira ya saa 3:00 asubuhi hadi saa 8 mchana.
   Katika hafla hiyo alisema mgeni rasmi atakuwa mkuu wa mkoa wa Lindi Bi Mwantum Bakari Mahiza.
   Mheshimiwa Mmbaga alisema serikali wilayani Liwale kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wameandaa siku maalumu ya kukutana na wenzetu wenye ulemavu kusikiliza kero zao na hatimaye kupata chakula maalumu kilichoandaliwa kwa heshima yao.
Pia aliongeza kusema ili kuweza kukamilisha zoezi hili amewaomba watanzania kuhudhulia ili kuweza kujumuika na watanzania wenzetu. 

Post a Comment

 
Top