0

Mwaandishi wetu
Baraza la madiwani Halmashauri ya  wilaya ya Kilwa mkoani Lindi limeanzimia kuchukua eneo la ardhi  hekari 800 zinazodaiwa kumilikiwa ya Shirika la mafuta na petro TPDC  kwa miaka 30 kinyume  na sheria.
Akizungumza  kwenye kikao hicho Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa Maimuna Mtanda   alisema kuwa shirika la mafuta la Taifa (TPDC) limekuwa likimiliki eneo kwa madai ya kupewa   kampuni ya Kilamko  kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha  Sement
Alisema kuwa  halmashauri  imefanya jitihda ya kufutilia  usajili wa kampuni ya Kilamco ambayo  ilikuwa ina miliki eneo hilo  kwa msajili wa makampuni breella, lakini alipofika huko uongozi ulimueleza kuwa hakuna kampuni iliyosajiliwa kwa jina hilo.
kwa  kweli  ofisi yangu kupitia   idara ya ardhi tunaendelea  kufutitilia ili kupata ukweli wa mmiliki wa halali kati ya shirika la Mafuta na Petroli na Kilamko”alisema Mtanda .
Mtanda alisema  shirika la Taifa la mafuta. petroli walikuwa wanaushirkiano wa kikazi, na kampuni hiyo na kuchukuwa ardhi hiyo kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda miaka 30 iliyopita.
Naye Diwani wa kata ya Mitole Rafii Kuchao alisema kuwa kodi ya halmashauri inapotea ya shs bil.3 mpaka sasa tangu eneo hilo limechukuliwa bila kundelezwa
Kuchau alisema kuwa TPDC  ni tatizo kwa hiyo vyombo vya ulinzi na usalama vitumike kuweza kupatikana kwa kodi hiyo ya shs.bil 3  za kodi ya ardhi ili ziweze  kusaidia, miradi  mbalimbali ya maendeleo , wilayani humo.
Aidha Mwaka  2014   kulifanyika vikao vya baraza la madiwani halmashauri na uongozi wa shirika la Taifa la  mafuta na Petroli (TPDC) walikubaliana kwa pamoja kugawana ardhi ya hekali 800 kwa kila mamlaka ipatiwe hekali 400.
Hata hivyo halmashauri hiyo ilikataa pendekezo hilo na kuwataka TPDC kuandaa kikao cha makubaliano  ili waweze kujadili suala hilo na kulitafutia ufumbuzi

Post a Comment

 
Top