Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema
maiti zilizotambuliwa na zile zilizobakia, walipohesabu waligundua idadi
yao kufikia 50.
“Tumebaini kuwa maiti katika ajali ile zimefikia
50 baada ya kuhesabu vizuri zile zilizotambuliwa na ambazo bado
hazijatambuliwa hadi sasa,” alisema Masenza.
Awali, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Robert Salim
alisema majeruhi waliopokewa hospitali hapo walikuwa tisa na mmoja
ndiye amefariki dunia.
Alisema majeruhi huyo ni Osward Mwinuka (58), aliyefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa.
Dk Salim alisema hali za majeruhi wanne waliolazwa
Hospitali ya Rufaa ya Iringa zinaendelea vizuri wakati wengine wanne
hali zao siyo nzuri na wanatarajia kuwapa rufaa kwenda Hospitali ya
Taifa ya Muhimbili (MNH).
Alisema maiti waliofikishwa hospitalini ni 27 na nane walitambuliwa na kuchukuliwa na ndugu zao wengi wao kutoka Mbeya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi
aliwataja waliotambuliwa kuwa ni Mbezi Deogratius, mkazi wa Soweto
Mbeya, Editha Ngunangwa, mkazi wa Soweto, Mohamed Juma, mkazi wa Mbeya,
Ndenya Sixbert, mkazi wa Mbeya, James Kinyamaguho, mkazi wa Morogoro,
Said Halfan na Abuu Mangula.
Waliojeruhiwa ni Mustafa Ally, Dominic Shauri,
Tito Kyando, Martin Haule, Ipyana Mbamba, Fadhil Kalenga, Mussa Mwasege,
Nehemia Mbuji, Josam Abel, Tumpate Mwakapala, Nico Hamis na Esther
William.
Wengine ni Peter Mwakanale, Kelvin Mwakaladi,
Raphael Nerbot, Maga Sebastian, Catherine Mwijungu, Lucy Mtanga, Debora
Vicent, Ester na mwanaume ambaye jina lake halikuweza kujulikana
kutokana na kuwa katika hali mbaya.
Vilio mkoani Mbeya
Wakati huohuo, mitaa mbalimbali ya Jiji la Mbeya jana ilijaa misiba iliyotokana na ajali hiyo.
Waandishi wa habari ambao wamepoteza ndugu zao ni pamoja na
mwanahabari wa Kampuni ya Mwananchi Communications mkoani hapa, Brandy
Nelson aliyefiwa na kaka yake, Osward Mwinuka na mfanyakazi wa Kampuni
ya New Habari, Mercy Mwalusamba wa mkoani Iringa aliyempoteza mdogo wake
aliyetajwa kwa jina la Omega Mwakasege, wakati Tumaini Msowoya wa
gazeti la Uhuru wa Iringa akimpoteza kaka wa mumewe.
Taasisi zingine zilizoathiriwa na ajali hiyo ni
pamoja na vyuo hususani Chuo cha Maendeleo ya Jamii Uyole (wanne) Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam kinadaiwa kupoteza wanafunzi watano.
Baadhi ya misiba hiyo ilihusisha wanandugu zaidi
ya mmoja, wakiwamo wafanyabiashara, Alfred Sanga wa Soweto, ambaye
amefariki dunia na mdogo wake, Luteni Sanga.
Post a Comment