0


Na Frank saidi Lindi :

WANANCHI wa kijiji cha Kitohavi,kata ya Matimba, wilaya ya ya Lindi vijijini,wamemzuia mwanasheria wa Halmashauri ya wilaya hiyo,Nyamande Kazimil,kumuapisha Rashidi Abdallah Naveti (CCM) kuwa mwenyekiti wao,kwa madai hawakumchagua katika uchaguzi wa Serikali za mitaa uliopita.
Habari kutoka kijijini humo na kuthibitishwa na baadhi ya wasimamizi wa uchaguzi huo,na uongozi wa Halmashauri hiyo,zinaeleza tukio hilo, limefanyika Ofisi ya kata hiyo,mwishoni mwa wiki iliyopita.
Wakizungumza na mwandishi wa gazeti hili kijijini hapo,baadhi ya wakazi hao,Isumaili Juma,Ashura Selemani na Kindamba Kaisi kwa nyakati tafauti walisema katika uchaguzi wa serikali za mitaa  uliopita waliomchagua mgombea wa Chama cha wananchi (CUF) Rashidi Kionjo kuwa kiongozi wao.
“Katika uchaguzi huo sisis tumemchagua Kionjo wa (CUF) kuwa mwenyekiti wetu,lakini siku ya kuapishwa limepelekwa jina la Rashidi Naveti wa (CCM) hapo ndipo tusipokubali kuletea kiongozi tusiemchagua”Walisema wakazi hao.
Aidha,walisema siku ile ya upigaji kura uliofanyika mwishoni mwa mwaka uliopita,msimamizi msaidizi wa uchaguzi huo,Abdallah Ngoleka alimtangaza Rashidi Kionjo wa (CUF) kuwa ni mshindi katika uchaguzi huo kwa kupata kura (60) na kumshinda mpinzani wake,Rashidi Naveti wa (CCM) aliyepata kura (44).
Pia,wakaeleza katika uchaguzi huo,wagombea wote wawili wa (CUF) na (CCM) Waliweka saini zao katika Fomu ya matokeo wakiyakubali  matokeo ya uchaguzi huo,huku nyingine zikibandikwa kwenye mbao za matangazo zilizopo katika Ofisi hiyo ya serikali ya kijiji.
“Wagombea wote waliweka saini zao kuyakubali matokeo hayo, chakushangaza siku ya uapishaji limepelekwa jina la Rashi Naveti wa (CCM) ambae hakushinda katika uchaguzi ule”Alisema  Kionjo ndiye ali
Aidha,walisema kutokana na mtafaruku huo,mwanasheria huyo aliwaapisha wenyeviti wa vijiji vya Likwaya, Moka, Matimba, Kikomolela,Komoro na Makumba,wakiwemo na wenyeviti wa vitongoji na wajumbe.
Wakizungumza kwa nyakati tafauti na gazeti hili,mgombea Rashi Kionjo wa (CUF) alisema anachotambua yeye ndiye mwenyekiti mpya wa serikali ya kijiji hicho,baada ya kupata ushindi wa kura (60) zidi ya (44) za mgombea wake wa (CCM) Rashidi Navet.
Hata hivyo,mwanasheria huyo alipofuatwa na mwandishi wa gazeti hili,ili kupata kauli yake hakuwa tayari kutoa ushirikiano na kumtaka aende kuonana na uongozi wa halmashauri ya wilaya hiyo.
Mwandishi wa Gazeti hili alipofika Ofisi ya Halmashauri hiyo,ili kupata kauli ya mkurugenzi mtendaji wake,Oliver Umberto Vavunge,alijibiwa na sektari wake kuwa yupo kwenye kikao,hivyo ni vigumu kuweza kumpata kutokana na kutingwa na majukumu ya kikazi.
Zoezi la uhapishaji lilikuwa lifafanywe wiki iliyopita kwenye ukumbi wa Ofisi ya kata ya Matimba,na mwanasheria wa Halmashauri ya wilaya hiyo ya Lindi vijijini,Nyamande Kazimil.
Gazeti hili limefanikiwa kupata baadhi ya Fomu za matokeo ya uchaguzi huo,ambazo zinaonyesha watu 126 walijiandikisha kupiga kura,ambapo 124 walijitokeza kutekeleza zoezi hilo,huku mgombea wa (CUF) akipata kura (60) na wa (CCM) ikiambulia (44) tisa zikiharibika,hata hivyo takwimu hizo zinaonyesha utata kwani kura (11) hazijuikani ziliko

Post a Comment

 
Top