0


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiHxdruK1AciDPDnQegJrlsknV_Jpeg98kpzf_NsDCKiE38W4X1FC9g3pbvFdmZ7sxWCML6BjTwlnP05tqB11yYXbXUUJQBGyu_In1ZdfZTjkvXwxNgnbGVc7gPQC7cMpsuxlTRWbtE3lg/s1600/1.jpg
Na Mwaandishi Mtwara
Mkuu wa mkoa wa Mtwara Halima Dendegu, ameonesha kutoridhishwa na ufugaji wa  unaofanywa  katika shamba la kuzalisha mitamba ya ng’ombe lililopo katika ya wilaya ya Nanyumbu mkoa wa humo na kuahidi kuwatuma wataalamu wa mifugo toka ofisi yake ili wahainishe fursa zilizopo na namna ya kuboresha ili kukiwezesha kujiendesha bila ya kutegemea ruzuku ya serikali.
 Akizungumza na watumishi wa shamba hilo jana(jumamosi) wakati wa ziara yake ya kikazi aliyofanya wilayani humo mkuu wa mkoa huyo alionyeshwa kushangazwa  namna mifugo  wanavyofugwa kwa kutumia njia zisizo na ubora  hali ambayo ufugaji wa namna hiyo hautawaletea tija.
Alibainisha kuwa haoni sababu ya kituo hicho kuendelea kujiendesha kwa kutegemea ya  ruzuku ya serikali wakati kinauwezo wa kutumia fursa zilizopo kwa kuzalisha mitamba kwa wingi na kuiuza kwa wananchi ambao bado wanahitaji mitamba hiyo.
Alisema kuwa shamba hilo linafursa nyingi ikiwemo eneo zuri lenye nyasi na maji ya kutosha na kuwa  iwapo zitatumika vizuri zitawezesha kuboresha ufugaji na kuwa wenye tija na kuzisadia wilaya zinazotegemea shamba hilo kupata ngombe wa kufuga .
“Kwa kweli  kwa haraka nimeona zipo fursa nyingi hapa  lakini tatizo hamzitumii vizuri  hivyo nitawaleta wataalamu kutoka ofisi yangu ili waziahinishe na kuona namna zitavyosaidia kuleta tija”alisema Dendego.
 Alisema kwa kutumia fursa hizo zitakazoainishwa na wataalamu wa ofisi yake  atazishirikisha  halmashauri zote mkoani  kuona namna ya   kuchangia  katika kuboresha  shamba hilo ambalo ndilo tegemeo kubwa kwa wananchi wa mikoa ya Lindi,Mtwara na wilaya ya  Tunduru mkoa wa Ruvuma.
Kwa upande Meneja wa shamba hilo Issa  Hamisi Nambwalaja alisema kuwa ufinyu wa bajeti umesababisha shughuli nyingi za maendeleo kukwama  ikiwemo ununuzi wa ng’ombe  wazazi,ununuzi  wa trekta mpya na vifaa vya kuvunia na kufyekea wa vichaka na kuiomba serikali kupeleka kwa wakati.
 Alitaja  changamoto zingine zinazokabili shamba hilo lenye  ukubwa wa hekari 5633.7 ambalo lina uwezo wa  kutunza ng’ombe  2700 wa rika mbalimbali lakini lina ng’ombe 655 ni  pamoja na  uvamizi wa wakulima   ambapo wapo wanaolima na kurudi na wengine wamejenga vibanda ndani ya shamba

Post a Comment

 
Top