0

Viongozi wa halmashauri ya wilaya Nachingwea wakiwa kwenye kikao za baraza la madiwani
 
KUWA DC WA JK ATANGAZA KUTOGOMBEA  
Mwaandishi wetu,Nachingwea.
Februari 03:MWENYEKITI wa Chama cha mapinduzi {CCM} wilaya ya Nachingwea,mkoani Lindi,Albert Mnali,amevunja ukimya na minong’ono iliyokuwa ikiwasumbua wananchi kwa muda wakiwemo baadhi ya wanachama wa Chama hicho,kwa kuweka bayana kwamba hayupo tayari kugombea ubunge wa Jimbo hilo.
Kiongozi huyo wa kisiasa ametoa kauli hiyo,alipokuwa akizungumza katika mahojiano maalumu na timu ya waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali vilivyomtembelea nyumbani kwake mjini Nachingwea.
Mnali ambaye aliwahi kuwa mkuu wa wilaya mbalimbali  hapa nchini,ikiwemo ya kagera,kasha kufutwa kazi na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa madai ya kuwacharaza viboko walimu,amekanusha madai ya yeye kutaka kuwania nafasi ya ubunge katika Jimbo hilo la Nachingwea katika uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika mwaka huu.
Amesema kimsingi yeye hafikirii na hana mpango wa kutaka kugombea nafasi hiyo ya ubunge,kwani macho na mawazo yake ni kutaka kukioongoza Chama hicho hadi pale wanachama watakapoamua kumpumzisha kupitia  uchaguzi wa ndani ya Chama hicho.
Mnali akasema kwa sasa ni muda wa kupisha damu change kuongoza ili kuweza kukabiliana na changamoto za wakati huu,na yeye atabaki na kuendelea kuwa mshauri.
“Nadhani ni vema basi kupisha damu change ili ziweze kukabiliana na changamoto za wakati huu,kwani kwa mimi sasa natakiwa kuwa mshauri zaidi mshauri badala ya kazi za utendaji”Alisema Mnali.
Kiongozi huyo wa kisiasa ni miongoni mwa wanachama wanaotajwa kuwania kuomba ridhaa ya wananchi kutaka kugombea ubunge katika uchaguzi mkuu wa madiwani,wabunge na Rais unaotarajia kufanyika mwaka huu.
Wanachama makada wanaotajwa kuwania Jimbo hilo ambalo kwa sasa linashikiliwa na waziri wa mambo ya ndani,Mathias Chikawe,ni pamoja na mkuu wa wilaya ya Kilombero,Hassani masala,kamanda wa vijana (UVCCM) wilaya ya Nachingwea,Stepheni Nyoni,Katibu wa (CCM) wilaya ya Mkuranga,mkoani Pwani,Issa Mkalinga,mlezi wa Chipukizi wa wilaya hiyo,Gaston Owino Onyango.

Post a Comment

 
Top