0

PICHA KUTOKA MAKTABA

Mwaandishi wetuLindi….
Mtoto Farisi Yusufu Alife (15) mkazi wa Kiwanjani kata ya Nyengedi, Wilaya ya Lindi,amewashitaki kwenye baraza la kata  wazazi wake wawili kwa kutompeleka shule kwa ajili ya kuendelea na masomo yake ya kidato cha kwanza.
Akizungumza na mwandishi na timu ya waandishi wa habari waliotembelea kijiji hapo, mwanafunzi huyo Farisi Yusufu,alisema amechukua maamuzi hayo baada ya wazazi wake kutoonyesha nia ya kumpeleka shule ili kuendelea na masomo yake ya Sekondari.
‘’Ni kweli kwa mara ya kwanza nimewafikisha wazazi wangu wawili yaani baba na mama Baraza la kata kufuatia kutoonyesha niya ya kunipeleka shule,huku nikiwa nimefanikiwa kuchaguliwa kuendelea na masomo ya Sekondari kata ya Mtua ‘’alisema Farisi.
Mwanafunzi huyo alisema baada ya kuwafikisha katika Baraza hilo la kata na kutozwa faini y ash,10,000/-  na kupewa amri kuhakikisha wananipeleka shule mzazi wake hivi sasa yupo kwaenye maandalizi ya kumpeleka ili akaendelee na masomo yake.
Baba mzazi wa mwanafunzi huyo,Yusufu Alife amethibitisha kuwa yeye na mke wake Hadija Juma wamefikishwa katika Baraza hilo la kata kwa kosa la kutompeleka kijana wake kuendelea na masomo yake ya kidato cha kwanza.
’Nilikifikishwa mimi na mke wangu Hadija Juma,lakini baada ya kusikiliza maelezo ya mwenzangu ,Baraza likaona mzigo hule niubebe mimi na nikatozwa faini  ya sh.10000/- na kama ningeshindwa ilikuwa basi niende jela miezi mitatu’ alisema Alife.
Aidha,alitaja sababu zilizomfanya asimpeleke kijana wake huyo shuleni ni pamoja na hali ngumu ya kiuchumi inayomkabili ikizingatiwa ana motto mwingine anayemsomesha kidato cha tano shule ya sekondari Mahiwa.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Baraza hilo, Abdallah Malibiche,alikiri kuwa kijana huyo kuwafikisha wazazi wake hao baada ya kusikiliza maelezo ya pande zote mbili ndipo Baraza likaamua kumtia hatiani mzazi wa kiume na kumtoza faini  hiyo au kifungo cha miezi mitatu Jela.
‘’Mimi na wazee wenzangu wa Baraza baada ya kusikiloiza maelezo ya pande zote mbili yaani mtoto na wazazi,likaamua kumtia hatiani mzazi wa kiume kwasababu  ndiye kichwa cha nyumba na pia alikuwa akishauriwa na mke wake wampeleke shule kijana wao’’ alisema Malibiche.
Alisema shauri hiyo imepewa namba 02/BKN/2015, ambapo sababu zilizotolewa na wazazi hao kuwa na hali mgumu ya kiuchumi,umepingwa na Baraza hilo na kuamuru alipe faini ya sh.10000/-
Kwa upande Afisa Mtendaji wa kata hiyo ,Thomasi Ngomo amempongeza mwanafunzi Farisi Yusufu kwa uwamuzi huo na kuwataka watoto wengine kuiga  mfano wake katika kutafuta haki zao za kupata elimu.
‘’Taarifa uliyoisikia ndugu mwandishi ni ya ukweli kwani wote hao ni wazazi wa kata yangu hii ya Nyengedi kwa upande wangu nampongeza huyu kijana kwa maamuzi aliyoyafanya kwa wazai wake na ninawashauri watoto wengine kufuata nyayo hizo’’alisema

Post a Comment

 
Top