Na mwaansidhi wetu Kilwa
Wakulima wa
wilaya ya Kilwa, mkoani Lindi, wameiomba serikali kuharakisha mpango
wa upimaji wa Ardhi kupitia mpango wa matumizi bora katika maeneo
yao ili kuepuka migogoro ya wafugaji, wakulima na wawekezaji
kwani inasabisha kurudisha nyuma juhudi za kupambana na umaskini kwa jamii.
Ombi hilo limetolewa
kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji vya Njianne,Somanga,Kiwawa, Mipingoni
na Chang’ombe wilayani Ruangwa wakati walipokuwa wanazungumza na timu ya
waandishi wa habari waliotembelea katika wilaya hizo.
Mwenyekiti wa
serikali ya kijiji Miteja, wilayani humo Abrahamani Kachele anasema mpango wa
pekee utakaokuwa suluhisho lakupunguza migogoro ya ardhi
ni upimaji wa matumizi bora ya ardhi.
Kachele anasema
kutotengwa kwa maeneo maalumu ya wafugaji na
wakulima kumechangia kuwepo kwa kwa malumbano,migogoro
na vurugu za kila mara zilizosababisha uharibifu wa mazao ya wakulima na
mifugo. Anasema kuwa kwa mantiki hiyo hivyo ni vyema serikali ikaharakisha
zoezi hilo la upimaji,
“Ni vema serikali
ikatambua kuwa dawa pekee ya kuondoa migogoro ya ardhi kati ya
wafugaji na wakulima ni mpango wa matumizi bora ya
ardhi na ili mpango huo uweze kukamilika kwa
wakati ni vizuri kushirikisha wadau wate wanaoguswa na
hilo,” alisema Kachele.
Post a Comment