WATU
kadhaa wamejeruhiwa katika vurugu zilizotokea jana jioni huko Dumila
mkoani Morogoro kati ya wakulima na wafugaji ambapo polisi wameingilia
kati na kutumia mabaomu ya machozi kutuliza ghasia hizo.
Chanzo
cha vurugu hizo kinadaiwa kuwa ni kukatwa mkono kwa mkulima mmoja
aishiye Kijiji cha Mketeni wilayani Kiloasa wakati akibishana na mfugaji
ambaye ni kabila la Kimasai kuhusu eneo la kulishia mifugo.
Post a Comment