0



 Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Kilwa mkoani Lindi Ali Mtopa akizungumza na mwaandishi wa habari wa gazeti la raia Tanzania
mwaandishi wetu 
Kilwa......Wazazi na walezi  Mikoa ya Lindi na wametakiwa kuwasimamia  watoto wao kielimu  ili  kuepuka  kugeuzwa  vibarua  wa kufanya kazi ngumu  wakati wa uchimbaji wa  gesi utakapoanza.
Ushauri huo umetolewa na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Kilwa na mwenyeki wa chama cha mapinduzi mkoa wa Lindi Ali Mtopa  wakati alipokuwa anazungumza na timu ya waandishi wa habari waliotembelea ofisi kwake jana
  
Mtopa alisema wazazi wana wajibu mkubwa kuwasomesha vijana wao kwenda sambamba na mabadiliko ya kimaendeleo na fursa zinazo jitokeza katika mikoa ya kusini Lindi na Mtwara ambazo zinahitaji watu waliosoma.
Alisema uchimbaji wa gesi na mafuta, unahitaji kuwa na wafanyakazi waliosoma kama watoto hawatasomeshwa kikamilifu wataishia kufanya kazi ya kubeba mizigo na vibarua kwa ujira mdogo.
“nawaomba wazazi wezangu  tuwasimamie watoto wetu ili wasome vizuri,na tuache tabia ya kuwaoza umri mdogo tutawafanya kuwa vibarua” alisema Mtopa
Mtopa alisema kutokana na historia ya mikoa ya kusini hali ya kimaendeleo  iko nyuma iliyosababishwa  na ukosefu wa elimu hivyo ni jukumu la wazazi kusimamia elimu ya watoto ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanakwenda shule kwa wakati.
“Elimu ni msingi  wa kila kitu  na ukiwa na elimu utaweza kuepuka na matatizo ya ujinga ,maradhi na umaskini”. Alisema Mtopa.

Post a Comment

 
Top