0
tanki la kuhifadhia maji
kibanda maalumu cha mashine
                                             jamii ikiangalia miradi unapoendelea
(Diwani wa kata ya Mbaya bwana Ali kioi)



                                                                     Mashine


HATIMAYE TATIZO LA MAJI KWA WAKAZI WA KIJIJI CHA NAMIHU LAPATIWA UFUMBUZI,katika hatua nyingine ya kupunguza kama siyo kuondoa kabisa kero mbali mbali zinazoikabili jamii yetu ,wanakijji wa kijiji cha Namihu wilayani Liwale Mkoani Lindi wamepata neema ya kujengewa mradi mkubwa wa maji safi na salama kwa njia ya mtandao wa bomba mradi ambao umefikia hatuwa za mwisho katika ujenzi wake ambapo hapo jana wameanza kusukuma maji kutoka kwenye chanzo cha maji hayo hadi kwenye tanki lililojengwa kijijini hapo Namihu.Akiongea na mdau wangu wa makala hii diwani wa Kata ya Mbaya Mh.Alli N. Kioi alifafanuwa Kuwa mradi huu kwa sehemu kubwa umejengwa kwa fedha kutoka Benki ya dunia kama mfadhili ambayo ilitoa jumla ya fadha sh 281,000,000/= ambapo jamii iliweza kuchangia sh 3,500,000/= na kwamba mradi uliibuliwa katika ngazi ya kijiji na hatimaye ulifikishwa ngazi ya Halmashauri ya wilaya ambapo pia ulipata baraka na kuungwa mkono na mbunge wa jimbo la liwale Mh.Faith Mitambo.Mradi huu umekuja muda muafaka kufuatia tatizo la maji safi na salama ikiwa ni pamoja na upatikanaji wake kwa ujumla Kuwa mgumu hasa nyakati za kiangazi ambapo Mara nyingine wanakijiji waliweza hata kungojelea maji kwenye vyanzo vyake walifafanua wajumbe wa kamati ya maji ya kijiji hicho ambao walionyesha kuufurahia na kuhaidi kuuendeleza pindi watakapokabidhiwa rasmi.Aidha Mh Kioi aliendelea kufafanua kuwa mradi huu ni kati ya mitatu mingine miwili mmoja uko barikiwa na mwingine uko mpigamiti ambayo pia ipo katika hatua nzuri ya utekelezaji ,mradi huu wa kijiji cha Namihu unahusisha tenki ambalo linakadiriwa Kuwa na uwezo wa kuhifadhi maji yasiyopungua lita za ujazo 30,000 kwa wakati mmoja ambapo litahudumia wakazi wa kijiji hicho wasiopungua1250(kwa mujibu wa takwimu za mwenyekiti wa seriali ya kijiji).

Post a Comment

 
Top