0

wanawakeNa Tiganya Vincent-Dodoma
Mwenyekiti wa Wabunge  Wanawake wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anna Abdallah  ametoa wito kwa  wajumbe wanawake wa Bunge Maalum la Katiba kufanya kazi kwa ushirikiano katika kuhakikisha kuwa wanaweka maslahi ya mwanamke mbele katika uandishi wa Katiba mpya na sio vinginevyo.
 Mwenyekiti huyo ametoa kauli hiyo leo mjini Dodoma wakati anafungua semina ya siku moja  ya wajumbe wanawake wa Bunge Maalum la Katiba iliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake nchini (TAMWA)  kwa lengo la kuwaelimisha juu ya kuwepo  na haja ya kuwepo na vipengele vinavyotetea haki za wanawake na watoto katika masuala mbalimbali.
 Alisema kuwa wajumbe hao wanawanawake wanapaswa kuweka kando tofauti zao za kivyama, kiitikadi na kiimani na kuhakikisha kuwa haki za msingi zinaweka katika Katiba mpya itakayotunga ili kujenga usawa wa kijinisia katika masuala mbalimbali hapa nchini.
 
Anna Abdallah aliongeza kuwa ni vema wajumbe hao wakatumia fursa hiyo wliyoipata ya kuingia katika Bunge hilo maalum katika kuhakikisha kuwa vipengelea vinavyolinda haki za Wanawake na watoto na kupigania uwepo wa usawa wa asilimia hamisni kwa hamisi katika masuala mbalimbali.
 
Aidha aliongeza kuwa ni jukumu la wanawake wote walioko katika madaraka kuwatetea wanawake wengine ambao wako nje na hata kuwahamasisha kwa kuwapa moyo wa kuingia katika siasa na kuwania madaraka mbalimbali badala ya kuwakatisha tama.
 
Akitoa mada katika Semina hiyo Mkurugenzi Mttendaji wa TAMWA Valerie Msoka alisema kuwa ni vema wajumbe hao wakapigani wazi umri wa mtoto uwekwe wazi na pia umri wa kuweza kuoa na kuolewa.
 
Aliongeza kuwa mambo mengine ni pamoja na kuweka vipengele vinavyopinga ukatiili wa kijinsia kama vile kupinga ndoa za utotoni, ukeketaji , kulazimishwa biasha ya mapenzi na ubakaji.
 
Naye Makamu Chansela wa Chuo Kikuu cha Hubert Kairuki Profesa Esther Daniel alisema kuwa suala la uzazi salama ni muhimu likazingatiwa katika uandishi wa Katiba mpya ili kuzuia mimba za utotoni na vifo vinavyotokana na uzazi.

Post a Comment

 
Top