Image captionWaislamu duniani kote watakuwa kwenye mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani
Mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani unaanza wiki hii duniani kote, watu wenye imani ya dini ya kiislamu watajizuia kula chakula na kunywa tangu kuchomoza mpaka kuzama kwa jua.
Malengo haya ni katika kutimiza nguzo za uislamu kwa kuswali na kujizuia ,wakati kipindi hiki kikitazamwa kama nafasi ya kujisafisha kiroho.
Wakati kwa mtazamo wa kawaida linaonekana kama jambo rahisi, kuna imani chache na upotoshaji uliosabisha uwepo wa maoni tofauti kwa miaka mingi.
Yafuatayo ni mambo sita kati yao,sambamba na uchambuzi wa Shabbir Hassan, Mwanafunzi wa sayansi ya dini ya kiislamu na sharia, na Hafidh wa Koran, maana yake amehifadhi Korani yote
Miswaki
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionMswaki haubatilishi funga
Kusafisha meno hakubatilishi funga yako, kwa mujibu wa wasomi.
Hassan anasema mara chache watu hufunga wakiamini kuwa ladha ya dawa ya meno inatosha kubatilisha funga
Ingawa wasomi wengi wa maswala ya dini watakubalina kuwa kusafisha meno yako ni sawa, Bwana Hassan ana vidokezo kadhaa kwa wale walio na wasiwasi.
''Ushauri mzuri ni kutumia dawa ya meno kwa kiasi kidogo, tumia kitu ambacho hakina harufu kali.
Pia ameshauri kutumia miswaki ya miti yenye ladha ya asili, miti hii pia inaelezwa na shirika la afya duniani kuwa ni salama kwa matumizi ya mdomoni.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionKumbusu mtu kunaweza kubatilisha funga
Kumeza mate yako mwenyewe inaruhusiwa na pia inashauriwa kufanya hivyo
''madai haya hayana msingi kabisa, ameeleza Bwana Hassan, ''kumeza mate yako ni suala la asili halizuiliki hivyo halibatilishi funga.
Kitakachobatilisha funga ni kumeza mate ya mtu mwingine jambo ambalo linapaswa kuzuiwa
Hautaruhusiwa kumbusu mweza wako au mke wako,Mantiki nzima ya kufunga ni kudhibiti hisia, vikiwemo chakula, vinywaji na kuwa na wapenzi.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionWanaofunga Ramadani wanapaswa kuepuka kusengenya
Kula au kunywa si maswala pekee ambayo yataharibu funga
Maswala mengine yanahusisha ''Dhambi inayotekelezwa na ulimi'', alieleza Bwana Hassan, dhambi hiyo ni kama vile kusengenya, kujiapiza kwa watu wengine na kufitini.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionKula kitu bila kwa bahati mbaya hakuwezi kuharibu funga
Kama kweli ulisahau kabisa kuwa ulikuwa umefunga kisha ukala kitu, funga yako bado itahesabiwa kuwa halali, ilimradi tu uliacha mara moja baada ya kugundua.
Hata hivyo, kama kwa bahati mbaya umekula kitu katika mazingira ambayo yangeweza kuzuilika, kwa mfano wakati wa kutawadha kabla ya swala, basi funga yako ni batili.
moja kati hatua nane za kutawadha ni pamoja na kusukutua kinywa, kisha kwa bahati mbaya ukameza maji kutabatilisha funga yako.
Bwana Hassan anaeleza wakati wa kutawadha wakati umefunga, unatakiwa uepuke kusukutua, unashauriwa kuweka maji mdomoni na kutema mara moja.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage caption"Kama una tatizo la kiafya swali la kwanza kuuliza ni je,ninaweza kufunga?
Baraza la Kiislamu nchini Uingereza (MCB) lilitoa angalizo sambamba na shirika la kimataifa la afya ya macho wakiwataka watu kuendelea kutumia dawa kama vile za matone.
MCB pia imetoa mwongozo mwezi wa ramadhani kwa ajili ya matumizi ya hospitalini, ikieleza kuwa matone ya macho, sindano ni miongoni mwa tiba zisizoharibu funga.
Hata hivyo, kumeza dawa kutaharibu funga, inashauriwa kumeza dawa kabla na baada ya kufunga
Hassan anasema ''kwanza, kama una tatizo la kiafya,swali la kuuliza ni je ninaweza kufunga?
Koran inasema wazi kuwa usikilize ushauri wa Daktari''.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionWazee wenye umri mkubwa hawalazimiki kufunga
Katika uislanu, kufunga ni wajibu kwa wale walio na afya njema na wamefikia umri wa utu uzima, kwa kawaida miaka takribani 15.
Hii haiwahusishi watoto na watu walio wagonjwa, (kimwili na kiakili), wanaosafiri, waja wazito na wanaonyonyesha, kwa mujibu MCB.
Kuna njia nyingine watu wazima wanaoshindwa kufunga wanaweza kupata thawabu wakifanya, bila kujiweka hatarini
''Kama ni ugonjwa wa muda mfupi wanajua watapona basi watafunga siku nyingine, alieleza Bwana Hassan
Kama ni maradhi ya muda mrefu anaweza kutoa Fidia, mchango mdogo unaotolewa kwa siku, ambapo utakuwa ukilisha familia masikini
Kupitia safu yetu ya mahusiano, leo nimekuletea makala maalum hasa kwa wanawake kutokana na malalamiko ya wanawake wengi kuwapoteza waume zao. Ki...Read more »
kuzoeana baina ya wanandoa ni jambo zuri, kwa maana ya kila mmoja kumfahamu mwenzake, lakini kuzoeana huku kunaweza kuzalisha dharau hususani kwa...Read more »
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionHuenda ndege zikatengezwa bila madirisha katika siku za usoni.
Kampuni ya ndege ya Emirates imezindua nd...Read more »
Image captionMaandamano yamefanyika mjini Nairobi siku ya Jumatatu kulalamika kuhusu tuhuma za ubakaji katika shule ya Moi Girls Nairobi
Walimu pamoj...Read more »
Operesheni ya mwisho ya Tundu Lissu imefanyika na kumalizika salama.
Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), alifanyiwa op...Read more »
Haki miliki ya pichaAFPImage captionBado muswada unahitaji kupitishwa na Rais wa Rwanda Paul Kagame kabla ya kuanza kufanya kazi.
Bunge nchini Rwanda...Read more »
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania wasikubali kuchonganishwa na kwamba Serikali haiongozwi kwa misingi ya kidini bali imeziachia ta...Read more »
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.