0
Wasichana katika jamii ya Palek Sudan KusiniHaki miliki ya pichaNORWEGIAN REFUGEE COUNCIL (NRC)
Image captionWasichana katika jamii ya Palek Sudan Kusini
Ni miaka minne leo tangu kuanza kwa vita vya kiraia nchini Sudan kusini.
Ghasia hizo zimekuwa wimbi jeusi lililo zima matumaini yaliokuwepo yaliotokana na uhuru wa kujitenga na serikali ya Khartoum mnamo mwaka 2011.
Maelfu ya watu wameuawa na mamilioni wengine wameachwa bila ya makaazi.
Vita vilianza Sudan kusini baada ya rais Salva Kiir kumtuhumu aliyekuwa makamu wa rais Riek Machar kwa kupanga mapinduzi.
Kabila la Machar - Nuer - ambalo ni la pili kwa ukubwa katika nchi hiyo baada ya kabila la Dinka la rais Salva Kiir - lilitazama mzozo huo kama mauaji ya kimbari dhidi yao.
Wanachama wa kamisheni ya haki za binaadamu katika Umoja wamataifa nchini Sudan Kusini leo wanatoa ripoti ya utafiti wao wa siku mbili walioufanya katika jimbo lililopo kaskazini magharibi la Wau.
Wamekwenda kukusanya na kuhifadhi ushahidi wa ukiukaji wa aina yoyote na unyanyasaji wa haki za binaadamu na uhalifu unaohusiana na hilo.

Maisha hivi sasa kwa raia

Hivi leo bado hali ni ya kuogofya. Ni mvua kubwa tu ya msimu ndiyo inayositisha mapigano, angalau kwa muda.
Taifa limesambaratika - huku Umoja wamataifa ukionya kuwepo hatari ya kufanyika mauaji ya kimbari.
Roda ni mkulima Bangachor Sudan kusini, lakini ameshindwa kulilima shamba lake kutoka na ukosefu wa usalamaHaki miliki ya pichaNORWEGIAN REFUGEE COUNCIL (NRC)
Image captionRoda ni mkulima Bangachor Sudan kusini, lakini ameshindwa kulilima shamba lake kutoka na ukosefu wa usalama
Raia nchini humo wamekabiliwa na ubakaji, mauaji na katika baadhi ya maeneo - baa la njaa.
Miezi sita iliyopita, kuliitishwa msaada mkubwa kukabiliana na baa la njaa nchini.
Leo inakadiriwa raia milioni 4.8 bado hawapati chakula cha kutosha - ikiwa ni ongezeko la milioni 1.1 kutoka mwaka jana.
"Miaka minne tangu kuanza mzozo wa Sudan kusini, hali inazidi kuwa mbaya na matumaini ni finyu kwa hali kuimarika," amesema Rehana Zawar, Mkurugenzi wa shirika la wakimbizi Norway nchini Sudan kusini.
"Raia, wengi wao wanawake na watoto ndio waathiriwa wakuu wakati ghasia hizo zikiongezeka katika maeneo mengi ya nchi. Wakulima wanaogopa kushughulikia mazao yao, na wanawake wanakabiliwa na hatari ya kubakwa kila siku wanapokwenda kuteka maji na kukusanya kuni."
Uchumi umezorota. Jitihada za kuutatua mzozo zimeambulia patupu.
Wiki ijayo mazungumzo ya kutafuta kufikiwa makubaliano ya amani ambayo wengi wanayaona hayawezi kuokolewa - yanatarajiwa kufanyika katika mji mkuu wa Ethiopia Addis Ababa.
Lakini hakuna ishara ya vita hivyo vya kiraia kumalizika wakati wowote hivi karibuni.

Post a Comment

 
Top