Kamanda wa cheo cha juu anayehusika na masuala za nyuklia nchini Marekani, anasema atakataa agizo lolote lililo kinyume na sheria kutoka kwa rais la kutaka kutumika kwa silaha za nyulia.
Kamanda wa jeshi la wanahewa Jenerali John Hyten, anasema kuwa atatoa ushauri kwa rais na anatarajia kuwa suluhu la kisheria litapatikana.
Matamshi yake yanakuja siku chache baada ya maseneta nchini Marekani kujadili nguvu za rais katika kufanyika shambulizi la nyuklia.
Wengine walielezea wasi wasi kuwa rais Donald Trump anaweza kumairisha kifanyika shambulizi kama hilo.
- Korea Kaskazini inakaribia kuwa hatari kwa Marekani
- Korea Kaskazini yasifia jaribio jingine la nyuklia
Wengine hata hivyo walisema kuwa rais ni lazima awe na mamlaka ya kuamua bila ya mawakilia kuingilia kati.
Hii ni mara ya kwazna kikao kama hicho kufanyika kwa zaidi ya miaka 40.
Post a Comment