0
Huddersfield yailaza Man United katika mechi ya EPLHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionHuddersfield yailaza Man United katika mechi ya EPL
Huddersfield Town ilisitisha msururu wa Manchester United wa kutoshindwa huku kikosi cha Jose Mourinho kikilazimika kuwa pointi tano nyuma ya viongozi wa ligi manchester City katika uwanja wa James Smith.
United ilikuwa imefungwa mabao mawili pekee katika mechi nane msimu huu, lakini wakaongezwa mabao mawili katika dakika tano za mwanzo kufuatia makosa yalioadhibiwa na timu hiyo ya nyumbani.
Juan Mata alipeana mpira kwa makosa kwa Aaron Mooy katikati ya uwanja na baada ya kumpatia pasi nzuri Tom Ince, ambaye shambulio lake lilipanguliwa na David De Gea, raia huyo wa Australia alikuwa wa kwanza kurejesha mpira huo wavuni kutoka maguu 10 huku safu ya ulinzi ya United ikiangalia.
Baadaye beki wa Sweden Victor Lindelof aliyeingia kama mchezaji wa ziada kuchukua mahala pake Phil Jones aliyepata jeraha alizungukwa na Laurent Depoitre na kuongeza bao la pili kunako dakika ya 33.
Muurinho alifanya mabadiliko katika kipindi cha mapumziko akimuingiza Marcus Rashford na Herikh Mkhitaryan ambapo kijana huyo aliwapatia bao la kufutia machozi ikiwa zimebakia dakika 12 kupitia kichwa kizuri baada ya krosi ya Lukaku.

Post a Comment

 
Top