0
                                                   Mkuu  wa  mkoa  wa  TANGA   MARTIN  SHEGERA 
MKUU  wa  mkoa  wa  Tanga   Martin  Shegera Amewataka  waandishi  wa  habari  nchini  kufanya  kazi  kwa  weledi na  kujiendeleze  kielimu  ili  kukabilina   na  changamoto  za  kiutendaji na  sheria  za   mpya  ya vyombo  vya habari  nchini.

Shegera  alisema  hayo  kwenye  ufunguzi  wa  mkutano  mkuu  wa  mwaka  wa  umoja  wa  klabu  za  uandishi (UTPC) uliofanyika  kwenye  ukumbi  wa  Tanga  Beach.

Alisema serikali  inatambua  mchango  na umuhimu  wa  vyombo vya  Habari  nchini,  ya  kuelimisha, kusukuma maendeleo ,  na  kufichua  maovu  hivyo  ni  wajibu  wao  kutambua dhamani  yao  na kufanya  kazi  kwa  kuzingatia weledi.

Nae  Makamu  mwenyekiti  Jenny  Mihanji  aliomba  watendaji  wa  serikali  kutoa  ushirikano ili  waandishi  wa habari  waweze  kufanya  kazi  zao  kwa  uhuru na  Amani
Waandishi  wa  Habari  wakiwa  kwenye  mkutano  mkuu   wa  mwaka  UTPC TANGA  HOTEL

Post a Comment

 
Top