0

Jamaa wakiomboleza Baba Raghav DasHaki miliki ya pichaAFP
Image captionChanzo cha vifo hivyo hakijabainika

Watoto zaidi ya 60 wamefariki dunia katika hospitali ya umma kaskazini mwa India, maafisa wamesema, huku kukiwa na tuhuma kwamba huduma ya gesi ya oksijeni hospitalini ilikatwa kutokana na deni.
Maafisa katika jimbo la Uttar Pradesh wamekiri kwamba hakukuwa na oksijeni katika hospitali hiyo lakini wakasema vifo hivyo havikutokana na hilo.
Kulitokea wasiwasi katika hospitali hiyo, huku jamaa wakijaribu kuwasaidia wahudumu hsopitalini kutumia mifuko ya gesi kuwasiadia wagonjwa kupumua.
Wengi wa waliofariki walikuwa katika kitengo cha watoto wachanga au walikuwa wanatibiwa ugonjwa wa encephalitis.
Vifo hivyo vilitokea katika kipindi cha siku tano kuanzia JUmatatu katika hospitali ya Baba Raghav Das, katika wilaya ya Gorakhpur.
Watoto 30 walifariki Alhamisi na Ijumaa, hospitali hiyo imesema.
Afisa wa afya wa wilaya Anil Kumar amekiri kwamba kulikuwa na "suala kuhusu malipo" kati ya hospitali hiyo na kampuni inayowasambazia oksijeni, lakini akasema huenda vifo hivyo vilisababisha na mambo mengine kwani wagonjwa wengi waliolazwa humo walikuwa katika hali baya.

Baba Raghav Das HospitalHaki miliki ya pichaAFP
Image captionVifo vingi vilitokea katika wadi ya wagonjwa walio hali mahututi

Eneo hilo ni moja ya maeneo maskini zaidi India na hushuhudia vifo vingi vya watoto kila mwaka kutokana na maradhi ya aina nyingi, baadi kutokana na encephalitis.
Kumar alisema watapokea mitundi zaidi ya gesi wakati wowote kuanzia sasa, na pia kwamba wamelipa deni.
.

Baba Raghav Das HospitalHaki miliki ya pichaAFP
Image captionWafanyakazi walichunguza mitungi ya oksijeni hospitalini baada ya vifo hivyo kutokea


Post a Comment

 
Top