Kiungo wa Manchester City Yaya Toure amesaini mkataba mpya wa mwaka mmoja katika klabu hiyo ya ligi kuu.
Toure mwenye miaka 34 alijiunga city mwaka 2010 na amefunga magoli 81 katika michezo 299.
Mwanzoni mwa msimu huu, Toure aliachwa
nje ya kikosi kilichoshiriki michuano ya ligi ya mabingwa wa Ulaya na
kisha meneja wake Pep Guardiola akaingia kwenye malumbano na Dimitri
Seluk.
Kwa simu za hivi karibuni Toure
aliyejiunga na City akitokea Barcelona, ameibuka na kuwa muhimili wa
klabu hiyo jambo lililomfanya Guardiola kumuongezea mkataba mwingine.
Post a Comment