0


 Mkuu wa wilaya ya Liwale,mhe.Sarah Chiwamba akikaribishwa kukata utepe kwa ajili ya kumkabidhi ndugu Musa Mkoyage



 Mkuu wa wilaya ya Liwale,mhe.Sarah Chiwamba baada ya kukata utepe na kumkabidhi funguo ndugu Musa Mkoyage

ndugu Musa Mkoyage akiwa amebanda na kuliwasha trekta 
 Mkuu wa wilaya ya Liwale,mhe.Sarah Chiwamba akimpongeza ndugu Musa Mkoyage 
 Ndugu Musa Mkoyage akipongezwa na baadhi ya wafanyabiashara na wakulima walioudhulia hafla fupi hilyo
 Ndugu Musa Mkoyage akipongezwa na baadhi ya wafanyabiashara na wakulima walioudhulia hafla fupi hilyo
 Ndugu Musa Mkoyage akingoja kukabidhiwa trekta yake
Wa kwanza kutoka kushoto ni Meneja wa banki ya nmb huduma kwa mteja,Mwalimu Yesaya Mbwambo ,wa katikati  ni Ndudu Musa Mkoyage na wa mwisho Mkuu wa wilaya ya Liwale,mhe. Sarah Chiwamba. (Picha na Liwale Blog)


Banki ya NMB tawi la wilayani Liwale, mkoani Lindi  imeendelea  kuwahamasisha  wakulima kuongeza  uzalishaji zaidi  kupitia nchi ya viwanda  kwa  kumkopesha trekta 1,mkulima ndugu,Musa Mkoyage lenye thamani ya shilingi 68,500,000.

Akikabidhi trekta hilo leo juni 22,  Mkuu  wa  wilaya  wa Liwale,mhe. Sarah Chiwamba, alisema    kuwa hatua ya  kukabidhi  trekta  hilo ni  sehemu ya  utekelezaji  wa Ilani ya uchaguzi ya  Chama Cha Mapinduzi (CCM) na  kutimiza  dhana  ya  nchi ya viwanda .

Hivyo alisema  kuwa  wilaya ya Liwale ni moja kati ya wilaya ambayo  imekuwa  ikitegemea kwa    uzalishaji  wa  mazao ya  biashara ikiwemo korosho pamoja na chakula na  hivyo lazima  wakulima  kuendelea  kuhamasishwa  zaidi  ili  kujitokeza  kukopa  kwa Taasisi ya MNB ili  kuweza  kunufaika na  mkopo ili kuweza kumuunga mkono Rais juu ya kuweza kutimiza sera ya nchi ya viwanda.

Pia  Mkuu  wa wilaya  alitumia nafasi hiyo  aliwataka  wakulima walioudhulia hafla hiyo ya kumkabidhi trekta ndugu Mkoyage  ambaye amekopeshwa trekta  hilo  mbali ya  kutumia katika    kilimo cha  zao la korosho  pia  kuhakikisha  analima hata mazao ya  chakula  kwa  wingi  ili  kuendelea  kuongeza  uzalishaji wa mazao ya chakula katika wilaya ya Liwale.

Meneja wa banki ya nmb huduma kwa mteja,Mwalimu Yesaya Mbwambo  alisema  kuwa mkulima  huyo amejitokeza  kuchukua mkopo huo wa trekta jipya HP 60 ambapo banki imemkopesha asilimia 75 ya shilingi 68,500,000 kwa kuwa  alikuwa akinyanyasika  zaidi  kwa  kilimo  cha jembe la mikono hivyo kupitia trekta hilo sasa litaweza kumwongezea uzalishaji zaidi.

Meneja Mbwambo alisema mkopo huo wa trekta una riba ya asilimia 19 na muda wa kulipa mwaka hadi miaka 3 pia aliweza kulielezea sifa na vitu ambavyo zimeambatanishwa kwenye trekta hilo kuwa trekta ni jipya,lina nguvu kubwa ya HP 60,tela lake linauwezo wa kubeba tani 12 na inauwezo wa kubinua,lina four wheel Drive,majembe pamoja lina bima kubwa.

Kwa upande wake ndugu Musa Mkoyage mara baada ya kukabidhiwa trekta hilo alisema mkopo huo wa trekta utaweza kuleta tija katika kuweza kuondokana na kilimo cha jembe la mkono hivyo sasa ataweza kulima kwa wakati na kuweza kuongeza uzalishaji.

Mkoyage alitumia hafla hiyo kuwaomba wakulima walioudhulia kuweza kumunga mkono kushirikiana nae katika kuweza kuwahudumia kwenye mashamba yao pia aliwaondoa wasiwasi wakulima wezake kuondokana na dhana kuwa mikopo inakupelekea kwenye  matatizo aliwambia kuwa mkopo ni malengo na endapo mkopo utaubadilishia malengo au matumizi itapelekea kuyumba na kushindwa kurejesha mkopo na kutapata matatizo.


Akizungumza kwa niaba ya walima na wafanyabiashara walioudhulia kwenye hafla hiyo, Bwana Theophil Nnenjela aliipongeza banki ya NMB kwa kuweza kukopesha trekta hilo na sasa banki hiyo imefungua milango kwa wakulima kuweza kupata mikopo mbalimbali ili kuweza kujiinua kiuchimi na akiomba banki hiyo kutoa mikopo yenye masharti nafuu pamoja na riba ndogo.
 Ndugu Musa Mkoyage aliyekaa upande wa kushoto akiwa na Meneja wa banki ya nmb huduma kwa mteja,Mwalimu Yesaya Mbwambo
 Baadhi ya wakulima na wafanyabiashara walioudhulia kwenye hafla fupi ya kumkabizi ndugu Musa Mkoyage trekta iliyofanyika eneo la banki ya NMB wilayani Liwale.
 Baadhi ya wakulima na wafanyabiashara walioudhulia kwenye hafla fupi ya kumkabizi ndugu Musa Mkoyage trekta iliyofanyika eneo la banki ya NMB wilayani Liwale.

 Akizungumza kwa niaba ya walima na wafanyabiashara walioudhulia kwenye hafla hiyo, Bwana Theophil Nnenjela.

ANGALIA VIEO JINSI  MKULIMA ALIVYOFURAHIA KUPATA TREKTA HIYO

Post a Comment

 
Top