0

 WASHIRIKI WA MAFUNZO YA SERA YA GESI NA MAFUTA WAKIWA KWENYE KAZI ZA VIKUNDI

MWAANDISHI WETU

 Kukosekana   kwa  watendaji   wa wizara  ya  nishati na  madini     ngazi  ya chini , Halmashauri  na  Manispaa ni  miongoni  mwa sababu zinazochangia migogoro katika maeneo yanayochindwa  madini, gesi  na  Mafuta.
 
Hayo yamebainishwa kwenye  warsha ya  kuwajengea  uwezo wadau kuhusu Tasnia ya uziduaji wa gesi na asili yaliyoendeshwa na  Shirika na  Mrengo Correrition  kwa ufadhili  wa  shirika  la hifadhi na  kulinda  mazingira (WWF) yaliyofanyika   ukimbi  wa chama  cha  walimu Lindi.
 
Akizungumza  kwa  niaba  ya  washiriki  hao Mohamedi  Chimbuli  alisema kukosekana   kwa  wawakilishi   wa wizara ya nishati  na  madini  ngazi  za chini  ikiwemo wilaya kunachangia  kuweko  kwa migogoro hisiyo isha katika  maeneo ya  uchimbaji  kwa  kuwa  hakuna watendaji wakaribu   wanaoweza  kutatua tatizo  kwa  wakati.
 
Chimbuli  alisema kama  kutakuwa  na watendaji  wa  wizara  hiyo  ngazi  ya  wilaya  pamoja mchakato wa  kuomba  leseni ya  uchimbaji pia  ianze  ngazi  ya  vijiji hiyo  itasidia  kuondoa   migogoro  kati  ya  wawekezaji  na  wananachi.
 
Saidi Juma alisema elimu  na  uzalendo ni unahitaji  na  jambo  muhimu  kwa watanzania ili kuendesha raslimali za  nchi   kwa  maendeleo  endelevu.
Kwa  upande  wake  makamu  mwenyekiti  wa Mtandao wa  Mrengo Gottlieb Mpangala  alisema lengo  la  mafunzo  hayo  ni  kuwajengea  uwezo  wadau  mbalimbali kuhusu  masuala  ya ushawishi  na  utetezi  juu  ya  ufuatiliaji  mapato  na  matumizi ya  gesi   na  mafuta na  uchambuzi  wa  sera ya  gesi  na  mafuta Nishati  ya  mwaka  2015.
 
Mpangala  alisema mafunzo  hayo  yamekutanisha  watendaji  wa mitaa,maafisa mazingira,mashirika yasiyokuwa  yakiserikali,Madiwani   na  viongozi   wa  dini

 WADUA  WAKICHANGIA  MADA KWENYE MAFUNZO SERA YA  GESI NA  MAFUTA
 MKUU WA MKOA  WA  LINDI  GODFREY ZAMBI AKIWA NA WAFADHILI WA MRADI KAYA  MASIKINI TASAF

Post a Comment

 
Top