0
               Mwenyekiti wa viziwi mkoa wa Lindi, ndugu Jafar Murtaza.
 
Mwenyekiti wa viziwi mkoa wa Lindi, ndugu Jafar Murtaza  amewatakia kheri  waandishi wa habari katika siku ya kuadhimisha uhuru wa vyombo vya habari yanayofanyika  kimkoa katika kijiji cha Kiwalala jimbo la mtama mkoani Lindi. 

Murtaza  ameyasema hayo leo mei 3 alipokuwa akizungumza na Liwale Blogo kupitia mtandao wa kijamii.

Ndugu zangu waandishi nawaomba katika siku yenu ya  uhuru wa vyombo vya habari tufahamuni sisi ndugu zenu wa kutosikia (viziwi) hatupati habari kikamilifu na tunakata tamaa kufatilia kazi zenu kwasababu vyombo vyenu huwa havina wakalimani ambao ndio nguzo yetu muhimu.,ndugu waandishi ninyi ndio wapashaji habari piganieni haki zenu pia boresheni huduma zenu za utoaji habari kwa kuibua waandishi ambao ni rafiki wa wenye ulemavu wa kusikia yaani watafcri moja kwa moja. alisema Murtaza

 Pia aliwataka waandishi wa habari wasikubali kukandamizwa haki zao na wala kuingiliwa uhuru bila sababu za kimsingi pia awataka waandishi wa habari kuweka  vipaumbele kwa watu wenye ulemavu ili  wafuraie kazi za habari  na kuwaunga mkono kutokana na mchango wao wa kuwapatia habari.

Post a Comment

 
Top