Mwenyekiti wa Uwt wilaya Masasi Jubulei Sowani akimkabidhi
Jane Joseph Sabuni mgonjwa aliyelazwa wordi ya wanawawake na
watoto katika hospitali ya Ndanda wakati walipokwenda kusaidia
vifaa mbalimbali ikiwa ni moja ya kuhazimisha miaka 40 ya chama
cha mapinduzi
Na Fadhila Milanzi Masasi
Upungufu
wa damu katika Hospitali ya Ndanda
mkoani Mtwara imeelezwa kuwa ni moja
ya sababu inayochangia ongezeko la vifo
vya mama wajawazito na watoto
Hayo
yameelezwa na muuguzi wa wordi ya
mama wajawazito na watoto Renfrida
Hokororo wakati alipokuwa anazungumza na uongozi
wa umoja wa wanawake Ccm Wilaya ya Masasi
wakati walipokwenda kutoa misaada ya vifaa mbalimbali
katika wordi hiyo.
Renfrida
alisema tatizo la damu kwa mama wajawazito na
watoto katika hospitali hiyo ni kubwa
hivyo ni vyema wanawake na jamii kwa ujumla
ikaona umuhimu wa kuchangia damu ili
kuokoa maisha ya wanawake na watoto
Alisema
kuwa katika kipindi cha mwenzi januari
wanawake tisa walilazwa katika wordi hiyo
lakini mama mmoja alipoteza maisha baada ya
kukosa damu kutokana na banki ya damu
kukosa damu ya group lake.
‘Kwa
niaba ya uongozi wa hospitali ya natoa shukrani
kwa msaada mulioleta lakini niwaombe wanawake mwenzangu kuangalia
uwezekano wa kuchangia damu kwa ajili ya
kuokoa maisha ya watoto wetu na wanawake wezetu
wanaolazwa katika wordi hizi’ alisema Hokororo.
Velonica
Mmole muunguzi mkunga alisema kuwa kitendo kilichofanywa
na wanawake wa jumuhia ya wanawake wa chama
cha mapinduzi inastaili kuigwa kwani kimeonyesha
ualisimia wa matendo ya wanawake ya
kuhurumiana
Mwenyekiti
wa jumuhia ya wanawake wilaya Masasi (UWT)Jibulei
Sowani ameiomba jamii kuchangia damu ili
kuokoa maisha ya wanawake na watoto
ambao ni taifa la kesho
Alisema
ili kutengeneza taifa zuri la kesho
hakuna budi kila mmoja kuona umuhimu wa
kuwasaidia watoto na wanawake wajawazito
kwa kuchangia damu ili wajifungue salama
Sowani
aliongeza kuwa wanawake wilayani masasi wameguswa
na tatizo hilo hivyo watajipanga na kuangalia
uwezekano wa kuchangia damu kila inapohitajika
Aidha
viongozi na wananchama wa umoja wanawake wa chama cha mapinduzi
katika madhimisho ya kuzaliwa chma hicho walifanya
zoezi la usafi na kutoa msaada wa sabuni kwa wagonjwa hasa wakina mama na
watoto linapojitokeza
Post a Comment