BAADA ya timu yake kufanikiwa kukaa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu
Tanzania Bara Jumapili iliyopita kwa kuwaondoa watani zao Simba, kiungo
wa Yanga, Thaban Kamusoko, amesema kwamba itakuwa ngumu wao kuondoka
kwenye nafasi hiyo.
Kamusoko alisema kuwa uwezo na malengo ambayo walikuwa wamejiwekea
yametimia na sasa wanachohitaji ni kulinda wasiondoke kwenye nafasi
hiyo.
"Asante Mungu kwa kupata pointi tatu muhimu, na sasa tunaongoza ligi,
natumaini kwa neema na baraka za Mungu, tutaendelea kupambana kwa ajili
ya kuongoza mpaka mwisho wa msimu," alisema kiungo huyo raia wa
Zimbabwe.
Aliongeza kuwa kila mechi wanayocheza tangu msimu ulipoanza ni ngumu kwa
sababu hakuna timu inayokubali kupoteza mchezo kirahisi huku akisema
kuwa timu zote ni sawa.
Yanga imekaa kwenye uongozi wa ligi ikiwa na pointi 46 baada ya mechi 20
ikifuatiwa na Simba yenye pointi 45 na Azam FC wenye pointi 34 katika
nafasi ya tatu.
Post a Comment