POLISI wilayani Kalambo imewakamata viongozi tisa wa serikali ya kijiji
cha Serengoma wilayani Kalambo kwa tuhuma za kujinufaisha na Sh milioni
tano zilizolengwa kwa ajili ya wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya
masikini wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf III).
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Steven ametoa amri ya kukamatwa viongozi hao wakati yeye na wao wakiwa mkutanoni.
Mkuu wa Polisi wa Wilaya ametekeleza amri hiyo, watuhumiwa wamekamatwa muda huo huo.
Zelothe amewaagiza wakuu wa wilaya mkoani humo kuhakikisha watumishi wote wa umma waliosababisha matumizi mabaya ya fedha hizo kwa kuwaingiza wasiostahiki katika mpango huo, zikiwemo kaya hewa, wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.
Baada ya kusikiliza kero za wanufaika wa mpango huo, Zelothe alimwagiza Mkuu wa Polisi wilayani hapa kuwakamata viongozi hao tisa wa serikali ya kijiji cha Serengoma, wanaotuhumiwa kujinufaisha na fedha hizo.
Zelothe amempa Mkuu wa Wilaya siku moja ahakikishe watuhumiwa wote 50 wamekamatwa na washitakiwe mahakamani.
Amewataka wakurugenzi watendaji wa Halmashauri za wilaya za Kalambo, Nkasi, Sumbawanga na Manispaa ya Sumbawanga wahakikishe wanataalamu wao wanawasaidia wanufaika wa mpango huo ili watumie fedha wanazopata kwa manufaa.
"Serikali haitasita kuwachukulia hatua watakaonda kinyume na utaratibu,” alisisitiza.
Imeelezwa kuwa kaya 866 zikiwemo kaya hewa 195 zimeondolewa katika mpango huo mikoani Rukwa na Katavi wakati wa uhakiki uliofanyika kuanzia Februari hadi Oktoba mwaka jana.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Steven ametoa amri ya kukamatwa viongozi hao wakati yeye na wao wakiwa mkutanoni.
Mkuu wa Polisi wa Wilaya ametekeleza amri hiyo, watuhumiwa wamekamatwa muda huo huo.
Zelothe amewaagiza wakuu wa wilaya mkoani humo kuhakikisha watumishi wote wa umma waliosababisha matumizi mabaya ya fedha hizo kwa kuwaingiza wasiostahiki katika mpango huo, zikiwemo kaya hewa, wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.
Baada ya kusikiliza kero za wanufaika wa mpango huo, Zelothe alimwagiza Mkuu wa Polisi wilayani hapa kuwakamata viongozi hao tisa wa serikali ya kijiji cha Serengoma, wanaotuhumiwa kujinufaisha na fedha hizo.
Zelothe amempa Mkuu wa Wilaya siku moja ahakikishe watuhumiwa wote 50 wamekamatwa na washitakiwe mahakamani.
Amewataka wakurugenzi watendaji wa Halmashauri za wilaya za Kalambo, Nkasi, Sumbawanga na Manispaa ya Sumbawanga wahakikishe wanataalamu wao wanawasaidia wanufaika wa mpango huo ili watumie fedha wanazopata kwa manufaa.
"Serikali haitasita kuwachukulia hatua watakaonda kinyume na utaratibu,” alisisitiza.
Imeelezwa kuwa kaya 866 zikiwemo kaya hewa 195 zimeondolewa katika mpango huo mikoani Rukwa na Katavi wakati wa uhakiki uliofanyika kuanzia Februari hadi Oktoba mwaka jana.
Post a Comment