Mara nyingi inakuwa ni shida na tatizo kubwa kufanikiwa
kwa wajasirimali wengi wachanga au wanaoanza biashara zao na kuingia
katika biashara kwa mara ya kwanza, huku wakiwa wamejaa hofu na uoga
mkubwa wa kushindwa katika biashara zao wanazoazisha, hii ni kutokana na
wengi wao kuwa na uoga wa kuhofia kuishia njiani na kupoteza mitaji na
biashara zao na hatimaye kupata aibu kubwa kwa watu waliowazunguka.
Wapo wajasiriamali wengi walio na hofu ya kufeli katika biashara zao
hii ni kwa sababu ya maneno mengi waliyowahi kuyasikia kutoka kwa watu
waliokwisha kuwatangulia kwenye biashara hapo mbele, na wakati mwingine
yawezekana ni kutokana na watu wa karibu kabisa wanaowaamini kwa
mashauri kutoka kwao wamewapa ushauri wa kuwakatisha tamaa badala ya
msaada wa kuchukua hatua iliyo salama yenye matokeo chanya zaidi.
Inawezekana umewahi kusikia utafiti kama huu uliowahi kufanyika
nchini marekani, utafiti huu unasema kuwa; “kati ya asilimia 90% ya
biashara nyingi mpya zinazoazishwa zinafeli baada ya miaka 3 tu.” Kama
unakumbana na utafiti kama huu na ni mara yako ya kwanza unataka kuingia
katika biashara, uwe na uhakika unaweza kukata tamaa na hata kuacha
kutimiza maono yako ya kufanya biashara. Usiogope bali unachotakiwa
kufahamu ni nafasi yako unayotakiwa kuitoa ya kujifunza zaidi kila siku
ili kujua ni namna gani ya kuepukana na hofu ya kufeli hasa juu ya mambo
yote yanayokujengea hofu hiyo ndani yako.
Kuna sababu nyingi sana zinazosababisha biashara nyingi kufeli na
kuishia njiani, lakini nataka kukuambia sababu hizo zisiwe ni kisingizio
au mchango mkubwa wa kukufanya uogope kuendeleza au kufanya biashara
uliyokusudia. Kumbuka njia pekee ya kuepukana na uoga au hofu ya kufeli
na kushindwa ni kuamua kulikabili tatizo husika pasipo uoga wowote mbele
yako.
Warren Buffett bilionea mwekezaji anayetajwa katika tano bora ya mabilionea na matajiri wakubwa duniani ndani ya mtandao wa forbes
aliwahi kusema kuwa, “Warren Buffett said that he would not invest in
any business where the owner hasn”t failed at least twice. I love that
truly wealthy and successful people understand that failure is part of
the process.” Utawekeza vipi katika biashara ambayo haijawahi kupata
misukosuko mingi ya kufeli hata mara kadhaa, ni ngumu kujua njia za
mafanikio yake. Watu wengi waliofanikiwa wanaelewa na kujua kufeli ni
sehemu ya mafanikio ya jambo fulani. Kwa nini wewe unaogopa kufeli?
Hakuna mafanikio mazuri nje ya kuanguka au kufeli mara nyingi kama
unahitaji kujua na kujifunza zaidi ili kuwa bora.
Hapa kuna mikakati sita ya kukusaidia kuondokana na hofu ya kufeli kama wewe ni mjasiriamali mchanga katika biashara.
1: Elewa kwanza kufeli ni sehemu ya mafanikio yako.
Mojawapo ya sababu kubwa kwa nini watu wengi hasa kwa wajasiriamali
na wafanyabiashara wengi wanafeli katika biashara zao, hii ni kwa sababu
hawajajua au kuchukulia kufeli katika biashara au jambo fuani ni sehemu
ya mafanikio. Huwezi kukimbia kufeli kama unahitaji kufika katika
mafanikio makubwa unayoyataka, kufeli ni sehemu ya maisha ya mwanafunzi
anayetaka kujifunza na kujua mambo mengi zaidi ya wengine.
Jambo kubwa unalopaswa kulifamu na kulichukulia hatua katika eneo
hili, ni mwenendo mzima kutoka kwako binafsi wa kukubaliana na kufeli
kwako au kushindwa ili upate kujifunza zaidi na kutoweza kurudi katika
makosa kwa mara ya pili. Kufeli si sehemu ya matokeo hasi tu wakati wote
kama wengi wetu tunavyofikiri, bali kufeli kunaweza kuwa ni sehemu
mojawapo kubwa ya mafanikio yako. Kumbuka Thomas Edison alifeli mara
1000 katika kutengeneza taa (bulb) ya mwanga wa umeme, lakini
alipofuatwa na kuulizwa alikiri hakufeli bali alitumia njia elfu moja
alizopata kumfikisha katika mafanikio ya kutengeneza taa hiyo ya mwanga
wa umeme.
2: Acha kujilinganisha na watu wengine.
Kila eneo la biashara fulani au kampuni fulani inaweza kujifunza
kutoka kwa kampuni nyingine iliyoendelea kuzidi wao binafsi hasa kwa
ajili ya kuboresha na kuleta ubora na ufanisi wa kutosha katika eneo la
kazi. Hivyo hivyo kwa mjasiriamali au mfanyabiashara binafsi anaweza
kutumia mtindo huo ili kuboresha biashara yake na kuleta matokeo chanya
na makubwa katika biashara yake aliyonayo.
Unaruhusiwa kujifunza kutoka kwa watu wengine kwa kujipima kwa
kutumia eneo la uwezo na udhaifu wako wa kibiashara ulionao kutoka kwako
au kwa washindani wako, ila haurusiwi kujilinganisha kwa kutamani kuwa
kama wao kwa haraka katika biashara kwani huko ndiko mwanzo wa kuanguka
na kufeli kwako moja kwa moja. Wapo watu wanaoingia katika biashara
fulani na wakiona fulani kanunua mzigo mpya na yeye anataka kununua
mzigo mpya pasipo kuangalia biashara yake au stoo (stock) yake
inamruhusu. Hayo ndio makosa yanayoweza kukupelekea kufeli daima.
3: Chukua hatua ya kuendelea mbele kivitendo.
Jambo lingine linaloweza kukusaidia kuondokana na hofu ya kufeli
katika biashara kama mjasiriamali mchanga. Kama unatembea katika
wasiwasi, mashaka, uoga, hofu na mawazo hasi yanayokusumbua kwa muda
mrefu basi huo ndio wakati mazuri na maalum wa kuchukua hatua ya
kivitendo kwa ajili ya kuzikabili changamoto hizo zinazokuzuia kusonga
mbele kibiashara.
Kwa kukabili hofu na uoga wa kufeli au kushindwa kwa kuchukua hatua
za kivitendo, hii inakusaidia kukupa uzoefu na ufanisi wa kufanya kazi
zako kwa ubora na uanalifu mkubwa ukifahamu njia zote za kupita ili
kufikia mafanikio yako. Wajasiriamali waliofanikiwa wanatumia hofu ya
kufeli kama sehemu mojawapo ya kuwahamasisha kuchukua hatua za kivitendo
kwa ajili ya kufanikiwa katika biashara zao. Yawezekana ni hofu ya
kufeli, hofu ya kuchekwa au kushindwa, hofu ya umasikini, nakadhalika,
zote hizi ni vizuri uzitumie kama sehemu ya kukuhamasisha kufanikiwa
katika biashara yako na maisha yako binafsi.
4: Acha kuangalia tatizo, bali tafuta majibu ya tatizo husika.
Usijaribu kusahau kuwa biashara yoyote iwe inayotoa huduma au bidhaa;
kwa kupitia bidhaa au huduma hiyo inasaidia kuondoa shida na uhitaji
mkubwa uliopo katika jamii. Hivyo ni vizuri utumie matatizo
yanayojitokeza kama sehemu mojawapo ya fursa za kukusaidia kuongeza
ufanisi na ubora wa biashara yako na si kukimbia matatizo husika.
Kama wafanyakazi wako wanalalamikia matatizo yanayojitokeza katika
biashara yako, fahamu kuna fursa mpya mahali hapo; kama wateja wako
wanapata changamoto na tatizo kubwa la namna ya kupata bidhaa zako,
fahamu kuna fursa mpya mahali hapo; kama wasambazaji wa bidhaa zako
wanalalamikia ugumu wanaokutana nao katika kusambaza bidhaa zako, fahamu
kuna fursa mpya mahali hapo. Nataka kukuambia kwa kadiri changamoto
zinavyojitokeza katika biashara yako na kuzichukulia hatua ya kuziondoa
ndio kadiri unavyoiweka biashara yako katika ubora na muonekana mzuri wa
maboresho.
5: Baki katika mawazo chanya.
Jambo hili ni muhimu pia ulifahamu kama unahitaji kuona matokeo
makubwa kwenye biashara yako. Kama wewe ni kiongozi na meneja katika
biashara au kampuni fulani unahitaji kufahamu ni muhimu sana kubakia
katika mawazo chanya pasipo kutoka hata kama kuna mazingira hasi
yanayojitokeza na kutaka kukutoa katika msimamo wako mwema wa
kufanikiwa.
Suala la kubakia katika msimamo wenye mawazo chanya ni la msingi sana
kama unahitaji kufanikiwa katika biashara yako na kuona mafanikio
makubwa nje na ndani ya kampuni ya shirika lako binafsi. Usiogope
kupambana na changamoto ndogo zinazojitokeza kwa nje na kutaka kukutoa
katika msimamo wa kibiashara. Changamoto kama vile za kukosa wateja kwa
muda fulani; kuharibika kwa bidhaa; kunyang’anywa wateja wako; kusemwa
vibaya, nakadhalika. Usiogope mambo yote hayo bali baki chanya na
kutumia mambo hayo kama fursa ya kukupa hatua nyingine ya juu zaidi.
6: Anza kwa kidogo ulichonacho, ukihesabu mafanikio yako unayoyapata.
Njia mojawapo ya mwisho ya namna ya kuondokana na hofu ya kufeli
kwako wewe mjasiriamali mchanga. Jifunze kuanza kwa hicho kidogo
ulichonacho na kutumia mafanikio yale madogo unayoyapata kama hatua ya
ushindi na sehemu ya kukutia nguvu ili kusonga mbele zaidi. Watu wengi
wanaichukulia hatua hii kama sehemu ya kuzuia kupata mambo makubwa kwa
haraka, hapana; bali tunafanya hivi ili kukupa msaada wa kukujenga
katika kujua wapi unakotoka na wapi unakokwenda ili kujenga ufanisi na
ubora mkubwa zaidi katika kazi au biashara.
Mafanikio unayoyapata yanazaa mafaniko mengine. Hivyo hauna haja ya
kukimbia mafanikio madogo unayoyapata katika biashara yako kwa kutaka
mafanikio makubwa na ya haraka zaidi. Kubali mafanikio madogo
unayoyapata ili ufanikiwe zaidi kwa mafanikio makubwa mbele yako.
Namna gani ya kuondokana na hofu ya kufeli katika biashara kama mjasiriamali mchanga unayeanza?
Unaweza ukaacha komenti yako hapo chini kwenye eneo maalum la kukomenti.
Unaweza ukaacha komenti yako hapo chini kwenye eneo maalum la kukomenti.
Post a Comment