0


Mkuu wa mkoa wa mjini magharibi Visiwani Zanzibar Mh, Ayoub Mohammed ameeleza kufurahishwa na ushiriki wa wananchi wa mkoa huo katika kilele cha maadhimisho ya miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar, sherehe zilizofanyika kwenye uwanja Amani mjini Unguja.


        Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mhe. Ayoub amesema kuwa wananchi wa mjini magharibi wameonesha ushirikiano mkubwa na kuiunga mkono serekali ya awamu ya saba chini ya uongozi wa Raisi wa Zanzibar na mweyekiti wa baraza la mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein.
        Aidha ametoa pongezi zake kwa vyombo vya ulinzi na usalama nchini kwa kuendelea kusimamia sula zima la amani na utulivu nchini na kuhakikisha inaendelea kulindwa.
        Shamra shamra za miaka 53 ya mapinduzi matukufu ya Zanzibar zilianza December 31 mwaka jana na kilele chake kilikuwa Alhamis.

Post a Comment

 
Top